Taarifa za hapa na pale
Inga-Britt Ahlenius, Mkuu wa Idara ya UM ya Uchunguzi wa Makosa ya Udanganyifu na Ulaji Rushwa (OIOS) alikutana na waandishi habari wa kimataifa waliopo Makao Makuu na kuwazindua ya kwamba moja ya shuruti muhimu zilizowekwa kudhibiti bora utekelezaji wa shughuli za UM, miongoni mwa watumishi wa taasisi hii ya kimataifa ni kuhakikisha kunakuwepo uwazi kwenye utekelezaji wa majukumu yao ya kazi, na pia uwajibikaji unaoridhisha, hususan ilivyokuwa wafanyakazi hawa wanaitumikia taasisi maalumu ya kimataifa yenye mazingira yasio ya kikawaida na ya aina pekee.