Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM kuanzisha tena duru mpya ya mazungumzo ya Sahara ya Magharibi

UM kuanzisha tena duru mpya ya mazungumzo ya Sahara ya Magharibi

Duru nyengine ya mazungumzo ya kutafuta suluhu juu ya mzozo wa Sahara ya Magharibi inatarajiwa kukutana katika mji wa Manhasset, kwenye Jimbo la Long Island, New York kuanzia Januari 7 hadi 9, majadiliano ambayo yatasimamiwa na UM. Kikao cha safari hii kitafuata taratibu ya mikutano iliopita, kwa kulingana na hisia kuu ya wawakilishi wa Morocco na Chama cha Ukombozi cha Frente Polisario, ambao hupendelea mazungumzo yao yawe ya faragha.