Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Bintou Keita, Special rep wa SG DRC akimvalisha medali mmoja wa walinda amani wa UN kutoka China walikamilisha jukumu lao leo huko jimboni Kivu Kusini mashariki mwa DRC.
MONUSCO

DRC: Walinda amani wa UN kutoka China waondoka Kivu Kusini

Baada ya huduma ya ulinzi wa amani kwa zaidi ya miaka 20 huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO, walinda amani kutoka China, hii leo wameondoka kutoka kambi yao iliyoko nje kidogo ya mji mkuu wa jimbo la Kivu Kusini, Bukavu ambako walishiriki kwa kiasi kikubwa katika ujenzi wa miundombinu.