UN WOMEN: Takriban wanawake 10,000 wameuawa huko Gaza
Takriban wanawake 10,000 wameuawa huko Gaza tangu kuzuka kwa vita miezi sita iliyopita na mtoto mmoja anajeruhiwa au kufariki dunia kila baada ya dakika 10, yameonya mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo huku kukiwa na ongezeko la ghasia katika Ukingo wa Magharibi na wasiwasi wa kuongezeka kwa mzozo wa kikanda kufuatia makombora ya Iran kushambulia Israeli.