Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watoto wanatibiwa katika hospitali ya muda huko Mouraj, kitongoji kilichoko kusini mwa Ukanda wa Gaza.
© WHO/Christopher Black

UN WOMEN: Takriban wanawake 10,000 wameuawa huko Gaza

Takriban wanawake 10,000 wameuawa huko Gaza tangu kuzuka kwa vita miezi sita iliyopita na mtoto mmoja anajeruhiwa au kufariki dunia kila baada ya dakika 10, yameonya mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo huku kukiwa na ongezeko la ghasia katika Ukingo wa Magharibi na wasiwasi wa kuongezeka kwa mzozo wa kikanda kufuatia makombora ya Iran kushambulia Israeli.

Gari linaendeshwa kupitia vifusi huko Khan Younis.
© UNOCHA/Themba Linden

Wataalamu wa haki za binadamu wanalaani jukumu la AI kwa uharibifu unaofanywa na jeshi la Israel Gaza

Wakati Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akirejelea ombi lake la hali ya kujizuia kwa kiwango cha juu zaidi Mashariki ya Kati kufuatia shambulio la ndege zisizo na rubani na kombora la Iran dhidi ya Israeli, wataalam huru wa haki za binadamu wamesema madai ya utumiaji wa kijasusi wa akili mbemba au bandia kwenye maeneo ya Gaza unaofanywa na jeshi la Israeli umesababisha athari zisizo na kifani kwa raia, nyumba na huduma.

Mwanamke akiwa na mtoto wake mchanga akiwasikiliza wafanyakazi wa UNFPA katika kikao cha kuongeza uelewa kuhusu ukatili wa kijinsia katika Kituo cha One Stop katika Hospitali ya Sominé Dolo.
© UNFPA Mali/Amadou Maiga

Safari hatari na isiyo salama ya wajawazito nchini Mali

Aissata Touré, mwenye umri wa miaka 16, ndio kwanza amejifungua mtoto wake wa kwanza. Mama huyu ambaye naye ni mtoto, alikuwa na matumaini ya kjifungulia karibu na kijiji chao cha Ngouma nchini Mali, lakini mhudumu wa afya alimshauri aende hospitali kutokana na uwezekano wa kupata tatizo wakati wa kujifungua. Ilikuwa safari yenye changamoto na gharama kubwa.

UNICEF inafanya kazi na serikali ya Nigeria kuhakikisha kila mtoto anapata mazingira salama ya kujifunzia.
© UNICEF/Dawali David

Miaka 10 ya watoto kutekwa Chibok, bado hakuna mifumo ya ulinzi - UNICEF

Nigeria inapotimiza miaka 10 tangu tukio la utekwaji nyara la watoto wa kike 275 huko Chibok, kaskazini magharibi mwa taifa hilo, hadi sasa bado watoto 90 wamesalia mateka na nchi hiyo inasalia na kumbukumbu ya tukio linguine la wanafunzi wa shule kutekwa nyara jimboni Kaduna mwezi Machi mwaka huu, hali inayosababisha Umoja wa Mataifa kutoa wito mahsusi.

Sauti
2'58"