FAO: Zaidi ya dola mil 16 kuwekezwa kwenye misitu nchini Uganda
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limezindua mradi wa thamani ya euro milioni 15 sawa na dola milioni 16.29 unaofadhiliwa na Muungano wa Ulaya EU ili kusaidia sekta ya misitu ya Uganda kuchangia kwa uendelevu zaidi kwa uchumi na mazingira.