Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Watu wakiwa wamekusanyika nje ya Hospitali ya Al Shifa Gaza ambako kumepatikana makaburi ya halaiki
WHO

GAZA: Makaburi ya halaiki yaonesha waathirika walikuwa wamefungwa mikono - OHCHR

Ripoti za kutisha zinaendelea kuibuka kuhusu makaburi ya halaiki huko Gaza ambako waathirika wa Kipalestina wameripotiwa kuvuliwa nguo wakiwa wamefungwa mikono, jambo ambalo limezusha wasiwasi juu ya uwezekano wa  kuweko kwa vitendo vya uhalifu wa kivita huku kukiwa na mashambulizi ya anga ya Israel yakiendelea kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, OHCHR.

Nyumba za Bunge, London, Uingereza.
© Unsplash/Paddy Kumar

Mashirika ya ndege jiepusheni na uhamishaji wa waomba hifadhi kutoka Uingereza kwenda Rwanda

Wataalamu wa Umoja wa Mataifa leo Aprili 22 wameelezea wasiwasi wao kuhusu jukumu la mashirika ya ndege na mamlaka ya usafiri wa anga katika kuwezesha kuondolewa kinyume cha sheria waomba hifadhi nchini Uingereza kuelekea nchini Rwanda kwa mujibu wa Mkataba kati ya serikali ya Uingereza na serikali ya Rwanda, na Muswada wa ‘Usalama wa Rwanda’.

Francine na watoto wake watatu walilazimika kuondoka kijijini kwake kutokana na mzozo usiokoma mashariki mwa DRC. Sasa wanapokea msaada wa WFP katika kambi ya wakimbizi wa ndani huko Kivu Kaskazini.
© WFP/Michael Castofas

WFP DRC waomba msaada wa $Mil 425 kusaidia wakimbizi wa ndani

Wakati Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemorkasia Kongo DRC ikiripoti kuwa na zaidi ya wakimbizi wa ndani 738,000 kwa kipindi cha mwaka huu wa 2024 pekee kutokana na kuongezeka kwa machafuko, Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP limeeleza kuwa na uhitaji wa haraka wa dola milioni 425 ili waweze kuwasaidia wakimbizi hao wanaoongezeka kila uchao. 

Sauti
1'49"
Baraza Kuu lilipitisha azimio mwaka 2012 lililoipa Palestina hadhi ya kuwa nchi isiyokuwa mwanachama katika Umoja wa Mataifa. (faili)
UN Photo/Rick Bajornas

Hadhi ya Palestina ndani ya UN yafafanuliwa 

Je, itachukua nini kwa Palestina kuwa Nchi Mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa? Wakati Baraza la Usalama linashughulikia suala hilo wakati vita vya uharibifu huko Gaza vikiingia mwezi wake wa saba, tuliangalia hali ya sasa ya Palestina na kile kinachohitajika kuwa Nchi Mwanachama wa Umoja wa Mataifa.