Ukosefu wa maji unaua watoto wengi kuliko hata mabomu- UNICEF
Ukosefu wa maji safi na salama unaweza kuua watoto walio na umri wa chini ya miaka 5 mara 20 zaidi kuliko mabomu na risasi katika maeneo ya kivita.
Ukosefu wa maji safi na salama unaweza kuua watoto walio na umri wa chini ya miaka 5 mara 20 zaidi kuliko mabomu na risasi katika maeneo ya kivita.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa nchi wanachama wa Umoja huo ambazo bado hazijatia saini na kuridhia mkataba wa kimataifa wa kuondokana na mabomu ya kutegwa ardhini na vilipuzi, zifanye hivyo haraka ili hatimaye kuondokana na mabomu hayo yanayoua na hata kuacha binadamu na ulemavu wa kudumu.
Nchini Ufaransa, wanamichezo wa zamani wataalamu wa mchezo wa raga, kupitia taasisi yao ya Ovale Citoyen, wanatumia mchezo huo kama njia ya kujenga kujiamini na kuleta hali ya kijamii kati ya wakimbizi na watu waliotengwa.
Maafisa wakuu wa Umoja wa Mataifa wametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuongeza fedha za ufadhili wa mipango ya misaada kwa ajili ya mamilioni ya watu nchini Syria na ukanda mzima, ambao wanategemea msaada wa kuokoa maisha na na kuweza kujikimu baada ya miaka kumi ya vita.
Ilikuwa siku, wiki, miezi na sasa imeshatimia miaka 10 tangu kuzuka vita nchini Syria na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR linasema nusu ya raia wa nchi hiyo wamelazimika kufungasha virango na kukimbia huku jinamizi la vita hivyo likiendelea kuwaandama.
Wakati vita vya Syria vimetimiza muongo mmoja ulioghubikwa na madhila ya hali ya juu, mjumbe maalum wa Umoja wa Matyaifa nchini humo ameliambia Baraza la Usalama leo Jumatatu kwamba "Vita hivyo vitaingia katika historia kama vita vya vibaya zaidi na vilivyoghubikwa na kiza kikuu katika miaka ya hivi karibuniya hivi karibuni akimaanisha kwamba watu wa Syria kama waathirika wakubwa wa karne hii .
Baada ya muongo mmoja wa mapigano nchini Syria, bado taifa hilo limesalia matatizoni tena katikati ya janga la ugonjwa wa Corona, au COVID-19, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa hii leo akizungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani wakati mzozo wa Syria ukitimu miaka 10.
Ukatili dhidi ya wanawake umeendelea kukita mizizi na sasa unaanzia tangu ujanani na hivyo kutia hofu kubwa, limesema shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO katika ripoti yake na wadau iliyotolewa leo huko Geneva, Uswisi na New York, Marekani.
Hii leo ikiwa ni siku ya wanawake duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema janga la COVID-19 limefuta maendeleo ya miongo kuelekea usawa wa jinsia huku wanawake wakikumbwa zaidi na machungu, bado kundi hilo limesalia kuwa mstari wa mbele kwenye hatua dhidi ya janga la Corona.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema hali mbaya ya hewa inayoambatana na majira ya baridi kali yaliyoghubikwa na kumwagika kwa theluji nyingi Mashariki ya Kati, imeongeza zahma kwa mamilioni ya wakimbizi na wakimbizi wa ndani.