Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Syria

Baba na mwanae wakiwa wamebeba hema la familia kwenye kambi ya Kerama huko Kaskazini mwa Syria karibu na eneo la Bab Al-Hawa mpakani na Uturuki.(Maktaba)
UNHCR

Kutopitishwa azimio la Baraza la Usalama ni hatari kwa Wasyria 

Baada ya jana Jumanne nia ya Baraza la Usalama kupitisha azimio ambalo ningeruhusu uvushaji misaada ya kibinadamu katika kivuko cha Bab al-Hawa kwenye mpaka wa Syria na Uturuki kaskazini-magharibi mwa Syria ili ikaokoe maisha ya wananchi wa nchi hiyo ambao wamekuwa kwenye zaidi ya miaka 12 ya vita kukwama kutokana na Urusi kupiga kura ya turufu kulipinga azimio hilo lingerefusha operesheni hiyo kwa miezi tisa mbele baada ya kufikia ukomo juzi tarehe 10 Julai, hofu sasa ni kuwa matokeo yake yatakuwa maumivu zaidi kwa wananchi wa Syria. 

Sauti
2'6"
Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanasafirisha misaada kibinadamu kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi kutoka Türkiye kwenda kaskazini magharibi mwa Syria.
© UNOCHA/Madevi Sun Suon

Ujumbe wa mashirika ya Umoja wa Mataifa watembelea walioathirika na tetemeko nchini Syria

Ujumbe wa mashirika saba ya Umoja wa Mataifa umetembelea hospitali na kliniki zinazoungwa mkono na shirika lisilo la kiserikali la Misaada na Maendeleo la Syria au SRD, Kaskazini Magharibi mwa Syria na kujionea athari za tetemeko la Ardhi lililoikumba nchi hiyo wiki mbili zilizopita pamoja na kujionea usambazaji wa misaada iliyotolewa na Umoja wa Mataifa.

Sauti
2'28"
Chakula kinasambazwa kwa watu waliokimbia makazi yao baada ya tetemeko la ardhi huko Aleppo, Syria.
© Al-Ihsan Charity

Tunataka kuwafikia waathirika wote japo kuna kikwazo cha usalama katika baadhi ya maeneo - WFP Syria

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaendelea kupeleka na kusambaza misaada nchini Uturuki na Syria ili kusaidia walioathiriwa na matetemeko makubwa ya ardhi yaliyotokea Jumatatu wiki hii na kujeruhi, kuua maelfu na kuharibu miundombinu. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) lina lengo la kuwafikia watu nusu milioni katika nchi zote mbili ijapokuwa kuna changamoto za kiusalama katika baadhi ya maeneo.

Sauti
2'59"
Familia 16 zinaishi katika shule iliyoharibiwa nchini Syria.
UNOCHA

Idhini ya kuvusha misaada ikikoma Julai 10, Wasyria watakuwa hatarini zaidi - OCHA 

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya uratibu wa misaada ya kibinadamu, OCHA, imeonesha wasiwasi wake kuwa ifikapo tarehe 10 mwezi huu wa Julai,  kushindwa kuongeza idhini iliyowekwa na Baraza la Usalama la UN ya kuvusha misaada ya kibinadamu kutaongeza viwango vya mateso kwa raia ambavyo ambavyo havijaonekana katika kipindi cha miaka 10 ya mgogoro wa Syria.

Sauti
2'21"