Watoto milioni 222 sasa wanaishi katika mazingira ya majanga yanayoathiri elimu yao: UNICEF
Mfuko wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa kuhusu elimu kwenye maeneo yenye dharura na majanga, ECW umetoa ripoti ya kutisha hii leo ikidokeza kuwa idadi ya watoto wenye umri wa kwenda shule, ambao wameathirika na majanga na hivyo kuhitaji msaada wa kielimu imeongezeka kutoka milioni 75 mwaka 2016 hadi milioni 222 hii leo.