Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Syria

Katika viunga vya mji mkuu wa Mauritania, Nouakchott, bustani ya mapangaboi ya kuzalisha umeme kwa njia ya upepo  yanaonekana kwa mbali na ni jawabu sahihi katika kuwa na nishati rejelezi
UNDP Mauritania/Freya Morales

Safari ya kuanzia UNFCCC hadi COP25:

Mabadiliko ya tabianchi yanatokea. Joto duniani sasa hivi ni nyuzi joto 1.1 zaidi ya ilivyokuwa mwanzoni mwa mapinduzi ya viwanda, na tayari linaleta madhara makubwa kwa ulimwengu, na kwa maisha ya watu. Ikiwa kiwango cha sasa kitazidi, basi kiwango cha joto duniani kinaweza kuongezeka kwa nyuzi joto 3.4 hadi 3.9 kwenye kipimo cha selsiyasi katika karne hii, kiwango ambacho kinaweza kusababisha madhara makubwa zaidi na yenye uharibifu kwa tabianchi.

Wanawake wakiteka maji katika mradi wa maji uliofadhiliwa na shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Dolow nchini Somalia. IOM, WFP na mashirika mengine waliweze kusaidia mahitaij ya wakimbizi hao kutokana na mfu
WFP/Georgina Goodwin

Kuchangia CERF ni uwekezaji bora zaidi- Guterres

Kuwekeza katika mfuko wa dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF si tu kunafanikisha usaidizi wa kibinadamu bali pia ni kuwekeza katika kuboresha kazi za chombo hicho chenye wanachama 193, amesema Katibu Mkuu Antonio Guterres jijini New  York, Marekani hii leo wakati akifungua kikao cha ngazi ya juu cha kuchangia mfuko huo  ulioanzishwa mwaka 2006.

Wakimbizi waliofurushwa wakipika katika kambi ya Qah karibu na mpaka wa Urutuki.
IRIN/Jodi Hilton

Shambulio la makombora lasababisha raia 12 kuuawa Idlib, Syria UN yataka uchunguzi ufanyike

Mzozo nchini Syria unaendelea kuua na kujeruhi raia huku ripoti zikisema  ufyatuaji wa makombora kwenye kwa makazi ya watu wanaokimbia machafuko katika maeneo ya kaskazini magharibi siku ya  Jumatano usiku, umesababisha watu 12 kupoteza maisha na makumi wengine ikiwemo watoto kujeruhiwa, yamesema mashirika ya Umoja wa Mataifa ya misaada ya kibinadamu hii leo.