Bado tuna wasiwasi mkubwa wa usalama wa watu milioni 3 Syria:UN
Umoja wa Mataifa umesema bado unawasiwasi mkubwa wa hatma ya usalama wa takriban raia milioni 3 huko Idlib Syria ambako zaidi ya nusu ya watu wote wametawanywa na kuwa wakimbizi wa ndani kufuatia ripoti za kuendelea kwa mashambulizi ya anga katika eneo hilo.