Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Syria

Baba akiwa na mwanae kwenye kambi ya wakimbizi kutoka Syria nchini Jordan.
UNHCR/A. Eurdolian

Msimu wa baridi, madhila zaidi ya wakimbizi wa Syria nchini Jordan

Miezi ya msimu wa baridi kali ikinyemelea, ni kumbukizi nyingine ya madhila kwa wakimbizi wa Syria waliosaka hifadhi Jordan ambao wengi wao wanaishi katika mazingira magumu wakati huu ambapo inaelezwa kuwa juhudi za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR na wadau wake Jordan za kuwapatia vifaa vya kukabiliana na joto zinaonekana kuwa muhimu zaidi.  Taarifa zaidi na Siraj Kalyango.

Msafara wa wahamiaji wa Amerika ya kati ukipita Chiapas Mexico (2018)
IOM / Rafael Rodríguez

Uhamiaji uwe wa utu kwa kila mtu- IOM

Katika kuadhimisha siku ya uhamiaji duniani hii leo, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM, António Vitorino ametaka hatua zaidi na za dharura zichukuliwe ili kulinda kundi hilo ambalo kila uchwao linakumbwa na madhila kote ulimwenguni.

Wakimbizi kutoka Iran, Venezuela, Syria, Afghanistan na Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR
UNHCR/UNICEF

Mkataba wa kimataifa wa wakimbizi kupitishwa leo

Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, Baraza Kuu la chombo hicho litapitisha mkataba wa kimataifa wa wakimbizi na hivyo kusaidia kwa kiasi kikubwa wale wanaokimbia makwao na nchi zinazowahifadhi, ambazo mara nyingi ni zile maskini zaidi duniani. Siraj Kalyango na maelezo zaidi.