Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Syria

Moja ya mitaa huko Douma, eneo la Ghouta mashariki nchini Syria ambako mapigano yamesambaratisha maeneo ya makazi.
UNICEF/Amer Al Shami

Vita dhidi ya ISIL vyaingia awamu mpya:Voronkov

Hii leo kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, wajumbe wameelezwa kuwa ingawa yaonekana kuwa magaidi wa ISIL wamesambaratishwa baadhi ya maeneo, bado kundi hilo ni tishio kwa kuwa limeibuka na mbinu mpya za kusajili wafuasi wanaoweza kufanya mashambulizi ya hapa na pale.