Utukutu wa watu wazima waendelea kutesa watoto Syria- UNICEF
Mzozo wa Syria sasa ukielekea mwaka wa nane, bado mapigano yanazidi kushika kasi, watoto wakiwa hatarini zaidi na haki zao za msingi zikisiginwa na watu wazima wasiojali chochote.
Mzozo wa Syria sasa ukielekea mwaka wa nane, bado mapigano yanazidi kushika kasi, watoto wakiwa hatarini zaidi na haki zao za msingi zikisiginwa na watu wazima wasiojali chochote.
Hii leo kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, wajumbe wameelezwa kuwa ingawa yaonekana kuwa magaidi wa ISIL wamesambaratishwa baadhi ya maeneo, bado kundi hilo ni tishio kwa kuwa limeibuka na mbinu mpya za kusajili wafuasi wanaoweza kufanya mashambulizi ya hapa na pale.
Mwakilishi wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya upokonyaji silaha Izumi Nakamitsu amesema ushahidi zaidi wa matumizi wa silaha za sumu zilizopigwa marufuku nchini Syria ni sharti zipewe jibu la kutosha na Baraza la Usalama la umoja huo.
Vita na ghasia zilizotamalaki Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini hususani kwa mwezi wa Januria zimewabebesha gharama kubwa watoto, limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Tupate taarufa Zaidi na John Kibego.
Kwa miezi miwili sasa hakuna msafara wowote wenye misaada ya kibinadamu ambayo imewafikia raia walioko katika maeneo ya Syria yaliyozingirwa.
Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya kibinadamu na msaada wa dharura, Ursula Mueller, amesema hali bado ni tete nchini Syria kufuatia mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yaliyodumu kwa zaidi ya miaka saba sasa.
Umoja wa Mataifa una wasiwasi mkubwa juu ya ustawi wa maelfu ya raia wanaokabiliwa na mapigano wakati huu wa operesheni za kijeshi kaskazini-magharibi mwa jimbo la Aleppo nchini Syria.