Ukosefu wa usawa katika mgao wa chanjo ya COVID-19 ni tishio la kutokomeza ugonjwa huo- Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo amehutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa akisema ukosefu wa uwiano katika mgao na utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona, au COVID-19 ni tishio kubwa katika kutokomeza ugonjwa huo ambao hadi sasa umesababisha vifo vya watu milioni mbili duniani kote.