Syria: Kueleka miaka 13 ya mzozo, Guterres ataka suluhu ya kudumu ya mzozo
Miaka 13 inaelekea kutimu tangu kuanza kwa mapigano nchini Syria wakati huu ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres anazungumzia udharura wa kupatikana kwa suluhu ya kisiasa nchini humo huku akisisitiza ulinzi wa raia na hali mbaya ya kiutu inayokabili wananchi.