Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Makubaliano ya kihistoria ya kuhuisha amani Sudani Kusini yatiwa saini kati ya rais Salva Kiir (kulia) na kiongozi wa upinzani Riek Machar, pichani ewakishikana mikono mjini Addis Ababa 12/9/2018
UNMISS\Nektarios Markogiannis

Awamu ya pili ya majadiliano ya kuunda serikali mpya Sudan Kusini yamefanyika mjini Juba

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir na aliyekuwa naibu wake Riek Machar wamekamilisha majadiliano ya siku ya pili mjini Juba nchini Sudan Kusini huku viongozi hao wawili wakirejelea azma ya kufikia amani huku wakiahidi kukutana mara kwa mara kuelekea uundaji wa serikali ya mpya ya umoja wa kitaifa inayotarajiwa Novemba 12 mwaka huu 2019.

Sauti
2'43"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akiweka shada la m aua huko Christchurch New Zealand kuenzi waathirika wa shambulio la Machi mwaka huu.
UN /Mark Garten

Siku ya kimataifa ya waathirika wa matendo ya vurugu yanayotokana na dini au imani yaadhimishwa kwa mara ya kwanza.

Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya kuadhimisha waathirika wa matendo ya vurugu yanayotokana na dini au imani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ulimwengu unapaswa kupinga na kukataa wale ambao kwa mabavu na kwa uongo wanashawishi kujenga imani potofu, kuchochea mgawanyiko na kueneza hofu na chuki. 

Sauti
1'43"