Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Watu waliotawanywa na machafuko Sudan wakiwasili Sudan Kusini kupitia mpaka wa Joda
© UNHCR/Ala Kheir

Janga kubwa la kibinadamu linaendelea Sudan: UNHCR

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva Uswisi  mkurugenzi wa mawasiliano ya nje wa UNHCR Dominique Hyde amesema "Sasa, mapigano yanaongezeka katika kiwango na ukatili wa hali ya juu unaoathiri watu wa Sudan, na ulimwengu uko kimya kwa kashfa hii, ingawa ukiukwaji wa sheria za kimataifa za kibinadamu unaendelea bila kuadhibiwa. Ni aibu kwamba ukatili uliofanywa miaka 20 iliyopita huko Darfur unaweza kutokea tena leo kukiwa na umakini mdogo. Kwa sababu hiyo, karibu watu milioni 6 wamelazimika kukimbia makwao na zaidi ya milioni 1 wamekimbilia nchi jirani ambako pia hali ni tete.

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), Nicholas Haysom akihutubia waandishi wa habari jijini Juba kuhusu hali ya usalama nchini Sudan Kusini.
UNMISS/Gregório Cunha

Sudan Kusini: Hatua inahitajika sasa kwa ajili ya uchaguzi kwa wakati na wa huru na haki - Nicholas Haysom  Haysom

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), Nicholas Haysom ametahadharisha kwamba muda unazidi kuyoyoma kuelekea Sudan Kusini kufanya uchaguzi mkuu unaotarajiwa mwezi Desemba mwaka ujao wa 2024 lakini bado masuala muhimu ya kuufanya uchaguzi huo uende kama ulivyopangwa bila kuchelewa hayajakamilika.

Sauti
2'18"
Nyumba ya familia huko Terekeka, Sudan Kusini.
Picha: FAO/Albert González Farran

FAO yasaidia jamii ya Wavuvi Sudan Kusini kutengeneza mnyororo wa thamani

Mkuu wa Mpango wa umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS ambaye pia ni mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini humo Nicholas Haysom amefanya ziara maalum ya kutembelea visiwa vilivyopo katika kaunti ya Terekeka na kujionea utekelezaji wa miradi ya stadi za maisha inayoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO. 

Sauti
3'3"