Takriban watoto milioni 3 jimbo la Al Jazirah Sudan wako hatarini huku ghasia zikiongezeka: UNICEF
Kuongezeka kwa mapigano katika jimbo la Al Jazirah nchini Sudan kumeripotiwa kuwalazimisha watoto wasiopungua 150,000 kutoka makwao katika muda wa chini ya wiki moja, limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.