Ntahakikisha nawainua wasanii wakike Sudan Kusini: Abul Oyay
Abul Oyay Deng Ajak ni msanii wa uchoraji anavyoinua jamii yake hususan wanawake katika taifa changa zaidi Afrika, Sudan Kusini
Abul Oyay Deng Ajak ni msanii wa uchoraji anavyoinua jamii yake hususan wanawake katika taifa changa zaidi Afrika, Sudan Kusini
Ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umefanya ziara na viongozi wa dini kuwatembelea wakimbizi wa ndani walioko Nagero huko Tambura li kuweza kuwajengea matumaini lakini pia kusikiliza mahitaji yao.
Tumeishi hapa tangu miaka ya 1950 na katu hatujawahi kushuhudia mafuriko kama haya, amesema mkazi wa jimbo la White Nile nchini Sudan ambako mafuriko makubwa yamesababisha wakimbizi wa ndani kusaka hifadhi kwa wenyeji wao huku shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na wadau wakiendelea kusambaza misaada ya kibinadamu. John Kibego na maelezo zaidi.
Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR inaonesha kuwa jamii ya kimataifa imeitikia vema wito wa kuwajibika pamoja katika kusaidia wakimbizi kupitia mkataba wa kimataifa wa wakimbizi, GCR.
Je wafahamu Umoja wa Mataifa? Asili yake ni nini? Majukumu yake ni yapi? Ungana nasi!
Mvua kubwa zilizonyesha katika kipindi cha miezi 6 iliyopita nchini Sudani Kusini zimeathiri miundombinu ya barabara, madaraja na viwanja vya ndege huku zaidi ya wakazi 700,000 wa kaunti ya Maban jimboni Jonglei wakisalia wakiiishi bila kupata msaada wowote kutokana na eneo lote kujaa maji.
Licha ya kutiwa saini kwa makubaliano mapya ya amani nchini Sudan Kusini mwaka 2018, mapigano bado yanaendelea katika maeneo tofauti tofauti nchini humo ikiwemo mji wa Tambura jimboni Equatoria Magharibi na hivyo kukwamisha harakati za kufikisha huduma za matibabu na wakimbizi wa ndani kuzidi kutaabika.
Nchini Sudan Kusini wakati sasa milio ya risasi inaweza kuwa imepungua katika baadhi ya maeneo ya taifa hilo, jinamizi la vita vya wenyewe kwa wenyewe bado linawaandama hasa kwa kuzagaa kwa manbaki ya silaha za vita kama mabomu ya kutegwa ardhini na vifaa vingine vya mlipuko, ambavyo kwa mujibu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa inayochukua hatua dhidi ya mabomu ya kutegwa ardhini UNMAS ni tishio la kila siku kwa maisha ya wanawake, watoto na wanaume kwenye maeneo mbali mbali nchini humo
Wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo wamesema hatua ya viongozi wasomi nchini Sudan Kusini ya kuhamisha kinyume cha sheria fedha nyingi na rasilimali zingine za umma wanadhoofisha haki za binadamu na kuhatarisha usalama.
Kwa kutambua ukosefu wa usalama na uhaba wa maji unaowakabili wakimbizi wa ndani walioko Tambura nchini Sudan Kusini, walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini humo wameanzisha doria maalum ya kuwasindikiza wakimbizi hao kuteka maji maji ili kuwahakikishia usalama katika kusaka rasilimali hiyo adhimu