Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Taswira kutoka juu ya mafuriko katika kambi ya wakimbizi ya Alganaa kwenye jimbo la White Nile nchini Sudan.
UNHCR Video

Hatujawahi kuona mafuriko kama  haya Sudan- Mkazi White Nile

Tumeishi hapa tangu miaka ya 1950 na katu hatujawahi kushuhudia mafuriko kama haya, amesema mkazi wa jimbo la White Nile nchini Sudan ambako mafuriko makubwa yamesababisha wakimbizi wa ndani kusaka hifadhi kwa wenyeji wao huku shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na wadau wakiendelea kusambaza misaada ya kibinadamu. John Kibego na maelezo zaidi.
 

Sauti
2'2"
UNMAS wakitegua mabomu katika eneo la Equatoria mashariki nchini Sudan Kusini. Pichani ni eneo shambani ambako kilipuzi kimebainika
UNMISS\Nektarios Markogiannis

Mabaki ya silaha za vita yaliyozagaa Sudan Kusini ni tishio kubwa la usalama wa raia:UNMAS 

Nchini Sudan Kusini wakati sasa milio ya risasi inaweza kuwa imepungua katika baadhi ya maeneo ya taifa hilo, jinamizi la vita vya wenyewe kwa wenyewe bado linawaandama hasa kwa kuzagaa kwa manbaki ya silaha za vita kama mabomu ya kutegwa ardhini na vifaa vingine vya mlipuko, ambavyo kwa mujibu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa inayochukua hatua dhidi ya mabomu ya kutegwa ardhini UNMAS ni tishio la kila siku kwa maisha ya wanawake, watoto na wanaume kwenye maeneo mbali mbali nchini humo 

Sauti
2'11"