UNHCR na Kenya zakubaliana kuhusu mustakabali wa kambi za Kakuma na Dadaab
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR na serikali ya Kenya wamekubaliana juu ya mustakabali wa kambi za wakimbizi za Kakuma na Dadaab nchini humo kwa kuridhia kuunda kamisheni ya pamoja ya kutoa majawabu ya masuala ya msingi kuhusu hatma ya wakimbizi.