Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Ajaba Ombacha, kutoka SUdan Kusini  mwenye umri wa miezi 17 akipimwa iwapo ana utapiamlo uliokithiri.
© UNICEF/UNI375881/Ryeng

UNICEF Sudan Kusini yamletea nuru Adut aliyekuwa hoi taaban 

Utapiamlo uliokithiri au unyafuzi ni tishio kubwa la uhai kwa watoto nchini Sudan Kusini ambako shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kutambua hilo linachukua hatua na sasa mtoto Adut ambaye mwaka 2019 alikuwa hoi bin taaban sasa anatembea na baba yake anajivunia.

Sauti
2'
Kamanda wa kikosi cha UNMISS akizuru baadhi ya barabara zinazokarabatiwa nchini Sudan Kusini.
UN/Gregório Cunha

Asante UNMISS kwa kukarabati barabara kati ya Yambio na Mundri – Wananchi Sudan Kusini 

Wananchi wa Sudan Kusini wanaoishi katika maeneo ya Yambio na Mundri wameshukuru Umoja wa Mataifa kwa ukarabati wa barabara katika maeneo ya Jimbo la Equatoria Magharibi ambayo yamekuwa hayafikiki wakati wa msimu wa mvua, lakini Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS, kupitia kikosi chake cha uhandisi cha Bangladeshi sasa wanayarekebisha.

Sauti
2'43"