Msemo wa ‘mfundishe mtu uvuvi badala ya kumpatia samaki’ wadhihirika Sudan Kusini
Tumu ya uhandisi kutoka Thailand, HMEC, inayofanya kazi kwa pamoja na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani Sudan Kusini, UNMISS imepatia wakazi wa eneo la Yei mjini Juba mafunzo ya kilimo cha mazao ya chakula sambamba na mapishi kama njia mojawapo ya kujitegemea katika chakula.