UNICEF yataka wanafunzi wote wa Sudan kupata fursa sawa ya kufanya mitihani ya taifa
UNICEF imezitaka mamlaka za Sudan na pande zote zinazohusika katika mzozo unaoendelea kuhakikisha kuwa kila mwanafunzi wa Sudan anapata fursa ya kufanya mitihani ile ile inayotambuliwa kitaifa bila kujali mahali alipo, ikionya kuwa ukosefu wa usawa katika upatikanaji wa mitihani unaweza kuhatarisha mustakabali wa kizazi kizima.