Mafunzo ya UNIDO yainua maisha ya wavuvi Sudan Kusini
Kuwaondoa watu kwenye umasikini ni lengo la kwanza la Malengo ya Maendeleo Endelevu SDGs ya Umoja wa Mataifa, ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda UNIDO limeanza kuona matokeo chanya kwa wavuvi kupitia mafunzo wanayotoa kwa vikundi mbalimbali vya uvuvi nchini Sudan Kusini.