Wanasiasa wasomi Sudan Kusini wapora mamilioni ya dola na kuchochea ukiukwaji wa haki na machafuko:UN
Wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo wamesema hatua ya viongozi wasomi nchini Sudan Kusini ya kuhamisha kinyume cha sheria fedha nyingi na rasilimali zingine za umma wanadhoofisha haki za binadamu na kuhatarisha usalama.