Uganda itaendelea kuwa kimbilio la wakimbizi- Rugunda
Sisi ni kizazi cha kutokomeza njaaTunaweza kuwa kizazi cha kwanza kufanikiwa kutokomeza njaa, kama ambavyo tunaweza kuwa kizazi cha mwisho kuikoa dunia.
Sisi ni kizazi cha kutokomeza njaaTunaweza kuwa kizazi cha kwanza kufanikiwa kutokomeza njaa, kama ambavyo tunaweza kuwa kizazi cha mwisho kuikoa dunia.
Tanzania imetaka hatua za dhati zichukuliwe ili kuokoa hoja ya ushirikiano wa kimataifa ambao hivi sasa uko mashakani.
Tanzania itatumia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, kutangaza msimamo wake na chombo hicho chenye wanachama 193. Taarifa zaidi na Assumpta Massoi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema miaka ya 70 ya tamko la haki za binadamu duniani, haijawa tiketi kwa kila mtu kufarahia haki za msingi zilizoainishwa katika nyaraka hiyo.
Viongozi wa nchi na wakuu wa serikali leo wamepitisha azimio la kisiasa lenye lengo la kuchagiza hatua dhidi ya ugonjwa wa Kifua Kikuu, au TB unaosababisha vifo vya watu milioni 1.6 kila mwaka.
Umoja wa Mataifa na nchi zinazochangia kwenye operesheni za ulinzi wa amani wa chombo hicho leo wamekuwa na kikao cha ngazi ya juu kuangazia jinsi ya kuimarisha operesheni hizo.
Mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukianza leo, wakuu wa nchi na viongozi wa serikali wa nchi zinazochangia kwenye operesheni za ulinzi wa amani wanakutana kujadili jinsi ya kukabiliana na changamoto za ulinzi wa amani.
Mwanadiplomasia nguli ambaye amewahi kufanya kazi na hayati Mzee Nelson Mandela azungumzia upekee aliokuwa nao mwendazake huyo ambaye leo anaenziwa na UN
Pengo kubwa la usawa kati ya ustawi wa binadamu unarudisha nyuma maendeleo ya ustawi wa binadamu, imesema ripoti mpya kuhusu kipimo cha maendeleo ya binadamu, HDI, iliyotolewa hii leo mjini New York, Marekani na shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP.
Mjumbe Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Burundi Michel Kafando amehitimisha ziara yake ya wiki nzima nchini humo iliyomkutanisha na wawakilishi wa serikali, vyama vya siasa na mashirika ya kiraia ambapo amewachagiza washiriki kwenye awamu mpya ya mazungumzo ambayo yanatarajiwa kuitishwa mwishoni mwa mwezi huu yakisimamiwa na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Mwandishi wetu wa maziwa makuu Ramadhani KIBUGA ametutumia taarifa hii kutoka Bujumbura, Burundi.