Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Burundi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres (kushoto) na Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania baada ya mazungumzo jijini New York, Marekani.mwezi Septemba 2021 (Maktaba)
UN / Evan Schneider

Tumeomba mazungumzo na UN wasaidie hali Burundi ili kuandaa Tanzania  kuwarejesha wakimbizi - Rais Samia 

Tanzania ni moja ya nchi za Afrika mashariki ambazo zimekuwa kimbilio la wakimbizi kwa miaka mingi. Rais wa nchi hiyo Samia Suluhu Hassan alipozungumza na Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa alipokuwa hapa New York, Marekani anasema ni takribani miaka 50 kwa nyakati tofauti nchi yake imekuwa ikipokea wakimbizi na kwa sasa ameomba mazungumzo na mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo la kuhudumia wakimbizi UNHCR kusaidia katika nchi wanakotoka wakimbizi ili waweze kurejea akitolea mfano Burundi.

Audio Duration
2'57"
Maza, ng'ombe ambaye amebadili maisha ya familia maskini nchini Burundi
@UNICEFBurundi/2021/Hamburger

Ng’ombe mmoja aleta hakikisho la maisha kwa kaya maskini Burundi

Mtamba mmoja wa ng’ombe anaweza kuonekana si chochote kitu kwa wafugaji wabobezi lakini kwa Beatrice Nibogora na familia yake nchini Burundi, mtamba huyo akipatiwa jina Maza amegeuka lulu na ufunguo wa maisha yenye matumaini na kutimiza methali ya wahenga ya kwamba baada ya dhiki ni faraja. Hii ni baada ya mradi wa Benki ya Dunia na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kubisha hodi kunusuru kaya maskini.

Sauti
1'58"
Watoto wakiteka maji machafu katika mto karibu na nyumbani jimbo la Ruyigi nchini Burundi. Septemba 14, 2017
© UNICEF/UN0185046/Haro

Licha ya ahadi, Burundi yaendelea kukiuka haki za binadamu na kufunga malngo wa demokrasia: HRC

Tume ya Umoja wa Mataifa ya uchunguzi kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Burundi imesema licha ya ahadi za awali za Rais Évariste Ndayishimiye za kuboresha haki za binadamu nchini mwake na kurejesha utawala wa sheria, bado hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kutimiza ahadi hizo, huku jukwaa la kidemokrasia likiendelea kufungwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu ukitamalaki tangu Rais huyo achukue madaraka Juni 2020.

Sauti
3'32"