Ahadi lukuki kusaidia wakimbizi zatangazwa Geneva, Uswisi
Mkutano wa kwanza wa ngazi ya juu kuhusu wakimbizi umefunga pazia huko Geneva, Uswisi ukiwa na ahadi lukuki za kusaidia wakimbizi na jamii zinazowahifadhi huku ahadi nyingi zaidi zikijikita katika usaidizi wa muda mrefu hususan ujumuishaji.