Jinsi Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa SDG unavyolenga kubadilisha ulimwengu
Wiki ya ngazi ya juu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa 2023, Mkutano wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG) itashuhudia viongozi wa dunia wakikusanyika mjini New York tarehe 18 na 19 Septemba. Kusudi lao: kurudisha ulimwengu kwenye mstari kuelekea mustakabali wa kijani kibichi, safi, salama na wa haki kwa wote.