Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Sio tu kwamba mikoko inasaidia kuzuia kuendelea kwa mabadiliko ya tabianchi, lakini pia ina jukumu muhimu katika kupunguza athari zake.
The Mangrove Photography Awards/Shyjith Kannur

Haya ndiyo mambo ya kutarajia katika Wiki ya mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi barani Afrika 2023

Viongozi wa Afrika wanatarajiwa kukutana jijini Nairobi, kenya wiki ijayo kwa jaili ya wiki ya mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi, Mkutano wa kila mwaka ambao wanatarajiwa kujadili njia mbalimbali za kupunguza utoaji wa gesi chafuzi huku wakija na mbinu za mnepo wa kukabiliana na athari za hali ya hewa.

Amadou Jobe, mhamiaji ambaye alirejea Gambia kutoka Ulaya, akiangalia bahari ya Pasifiki kutoka pwani ya Gambia.
UN News/ Hisae Kawamori

Sitamani tena kuzamia kwenda Ulaya: Manusura kutoka Gambia

Kila mwaka maelfu ya wahamiaji kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Afrika hujaribu kufika Ulaya wakivuka bahari ya Mediterania kwa lengo la kwenda kusaka maisha bora lakini safari hiyo inaelezwa kuwa ni hatari sana kwani maelfu ya watu hufa maji au kutoweka. Evariste Mapesa anatupeleka nchini Gambia kusikia simulizi ya kijana ambaye chupuchupu apoteze maisha. 

 

Sauti
3'19"
Kina mama kutoka Kenya ambao wananyonyesha watoto wao, wakiwatumbuiza wageni kwenye uzinduzi wa wiki ya kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa kunyonyesha.
UN News/Thelmaa Mwadzaya

Unyonyeshaji wa watoto maziwa ya mama huimarisha afya yao na ya mama - Wanaharakati Kenya

Kulingana na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, watoto wanaonyonya maziwa ya mama pekee katika miezi sita ya mwanzo ya uhai wanapiga hatua nzuri za kiafya kama anavyoelezea Kasha Mutenyo kwamba, "umuhimu wa kwanza wa kunyonyesha ni kwamba afya ya mtoto inaimarika na haugui kila wakati. Sio ghali, ni salama na hauhitaji vifaa vyovyote kumnyonyesha mtoto. Pia inamsaidia mama kupanga uzazi.”

Sauti
6'58"
Koketso Mukubani akisimama nje ya Kituo cha Matibabu cha Sediba Hope huko Tshwane, Afrika Kusini. Anasema wanaotumia dawa za kulevya wanapaswa kujumuishwa kwenye mipango na utekelekezaji wa kinga, tiba na huduma dhidi ya VVU na Homa ya ini C.
© UNODC

Simulizi Yangu: Kuishi na Homa ya Ini aina ya C nchini Afrika Kusini

Koketso Mokubane, mwanaume huyu raia wa Afrika Kusini alibainika kuwa na Homa ya Ini C. Amesimama nje ya kituo cha matibabu cha Sediba Hope kwenye kitongoji cha Tshwane. Koketso anafanya kazi ya kwenye ofisi ya Mtandao wa Watu wanaotumia dawa za kulevya nchini Afrika Kusini. Hili ni shirika lisilo la kiserikali linalopata msaada kupitia ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabiliana na Dawa na Uhalifu, (UNODC) kwa lengo la kutetea haki za watu wanaotumia dawa za kulevya.