Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Paulina Ajello mfanyakazi wa WHO kitengo cha mawasiliano na ushirikishaji jamii akizungumza na wanajamii waelimishaji kuhusu Ebola.
Picha: WHO_Uganda/PhilipKairu

Jiji la Kampala laendesha kampeni ya kupambana na ugonjwa wa Ebola

Wakati huu ambapo hakuna mgonjwa mpya wa Ebola aliyesajiliwa katika mji mkuu wa Uganda tangu tarehe 14 Novemba, 2022 mamlaka ya afya ya Mji Mkuu wa Kampala kwa kushirikiana na Wizara ya Afya ya nchi hiyo hivi karibuni ilifanya kampeni ya siku saba kuelimisha umma ili kudumisha umakini wa watu na hatimaye kusaidia kumaliza mlipuko wa ugonjwa huo hatari duniani.

Elizabeth Maruma Mrema (kushoto) ambaye ni katibu mkuu wa CBD akihudhuria mkutano  wa COP15 huko Montreal nchini Canada
Picha: CBD

Upotevu wa bayoanuai unaweka rehani kizazi hiki na vijavyo: CBD Elizabeth Mrema

Mkutano wa 15 au COP 15 wa mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu bayoanuai, CBD unaendelea mjini Montreal Canada ukizikutanisha serikali kutoka kote duniani na wadau wengine muhimu kwa lengo la kuafikiana malengo mapya yatakayoiongoza dunia katika hatua za kubadili mwelekeo na kusitisha upotevu wa bayoanuai ambayo ni tegemeo la viumbe na mazingira ifikapo mwaka 2030.