Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Watoto wakimizi wakionesha kuunga kwao mkono shughuli za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR za kutokomeza usafirishaji haramu huko Wad Sharige Mashariki mwa Sudan.
© UNHCR/Osama Idriss

Simulizi Yangu: Kukabili usafirishaji haramu Malawi

Maxwell Matewere, mtaalamu katika ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuzuia uhalifu na madawa ya kulevya, (UNODC) nchini Malawi, amekuwa akiendelea na harakati zake za kukabiliana na usafirishaji haramu wa binadamu kwa zaidi ya miongo miwili. Leo hii anapatia mafunzo maafisa mbali mbali nchini Malawi kuzuia na kukabili uhalifu: mwaka huu pekee licha ya janga la Corona au COVID-19, ameweza kuokoa watu 300 waliokuwa wakumbwa na usafirishaji haramu sambamba na kukamata watu 31 wahusika wa uhalifu huo.
 

Zimbabwe: Rebecca mama wa watoto watano. Picha: WFP / Claire Nevill
WFP/Claire Nevill

Wanawake na wasichana na janga la COVID-19

COVID-19 imeongeza ukosefu wa usawa katika kila sehemu ya jamii, na hivyo kuongeza hatari ya makundi yaliyo hatarini, pamoja na wanawake na wasichana. Janga hili linaongeza hatari ya unyanyasaji wa kinjisia (GBV), inarudisha nyuma maendeleo ya kijamii na ya kiuchumi ya wanawake na wasichana na kutishia afya ya uzazi.

 

 

Shughuli za ununuzi kwenye duka jijini Dar es Salaam, Tanzania wakati huu ambapo kumeripotiwa kutangazwa kwa visa vya corona nchini humo.
UN News/ Stella Vuzo

Tanzania inavyokabili janga la corona

Ni miezi miwili na zaidi sasa tangu Tanzania itangaze mgonjwa wake wa kwanza wa virusi vya COVID-19.  Tangu tarehe 16 mwezi wa tatu mwaka huu mengi yamejiri nchini Tanzania kufuatia kuzuka kwa janga la ugonjwa huo unaoathiri dunia nzima.