Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Pakaza rangi ya chungwa! Angazia haki za wanawake na wasichana na kataa ukatili dhidi ya wanawake na wasichana.
UN Women

Ukatili dhidi ya wanawake ni fedheha kwa jamii zote:Guterres

Ukatili dhidi ya wanawake na wasichana ni ugonjwa wa kimataifa unaoleta fedheha kubwa katika jamii zote duniani . Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake maalumu kuhusu siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake ambayo huadhimishwa kila mwaka Novemba 25.

Nchini Niger kondoo zinakabiliwa na hatari ya ugonjwa wa PPR
©FAO/Andrew Esiebo

Ugonjwa wa PPR waua mamilioni ya kondoo, mbuzi na maisha ya wafugaji

Zaidi ya nchi 45 leo zimesisitiza ahadi yao ya kutokomeza ugonjwa wa PPR au tauni inayokatili Wanyama wengi wadogo kama mbuzi na kondoo ifikapo mwaka 2030. Kwamujibu wa shirika la chakula na kilimo FAO na lile la kimataifa la afya ya mifugo OIE, wakizungumza katika mkutano uliomalizika leo mjini Roma Italia, ugonjwa huo wa kuambukiza unaua mamilioni ya mbuzi na kondoo kila mwaka .