Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Watoto milioni mbili wanahitaji msaada nchini Uturuki.
© UNOCHA/Ahmad Abdulnafi

Siku 100 baada ya tetemeko Uturuki na Syria, mamilioni ya watoto na familia zao bado wanahaha: UNICEF

Siku mia moja baada ya kutokea kwa matetemeko mabaya zaidi ya ardhi katika historia ya hivi karibuni nchini Uturuki na Syria, mamilioni ya watoto na familia zao wanahaha kujenga upya maisha yao, huku watoto milioni 2.5 huko Uturuki na milioni 3.7 nchini Syria wakihitaji msaada wa kibinadamu unaoendelea limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.

Wanaume na wanawake wa kiasili wa Nuñoa huko Puno, Peru, wakisuka mavazi kulingana na nyuzi za alpacas..
SGP-GEF-UNDP Peru/Enrique Castro-Mendívil

Kufadhili mustakabali bora kwa wote: Mambo 5 ya kujua kuhusu jukwaa la ufadhili wa Maendeleo

Huku uchumi wa dunia ukiendelea kuathiriwa na mfululizo wa migogoro, maafisa wakuu wa Umoja wa Mataifa na wawakilishi wa serikali wanakutana kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani, katika jaribio la kubadilisha mfumo wa fedha wa kimataifa, na kurejesha ajenda ya maendeleo endelevu ya 2030 iliyokubaliwa kimataifamkwenye mstari unaostahili.

Mbu aina ya Aeded aegypti ambaye anaweza kusambaza zika, dengue au chikungunya
IAEA/Dean Calma

Je wafahamu ugonjwa wa chikungunya?

Ugonjwa wa chikungunya kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO ni ugonjwa unaonezwa na mbu jike aina ya Aedes aliyebeba virusi vya chikungunya. WHO kupitia ukurasa wake wa kuchambua magonjwa inasema kuna spishi mbili za Aedes zinasambaza ugonjwa huo ambazo ni Aedes aegypti na Aedes albopictus. Spishi hizi mbili zinaweza pia kusambaza magonjwa mengine yanayoenezwa na kama vile dengue. Mbu hawa hung’ata nyakati za mchana, ingawa wanaweza pia kung’ata asubuhi na alasiri.