Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Mtoto wa umri wa miezi mbili apokea cheti cha kuzaliwa mjini Accra,Ghana.
UNICEF/Frank Dejongh

Usajili wa kuzaliwa ni nini na una umuhimu gani?

Katika nchi nyingine, usajili wa kuzaliwa haupewi kipaumbele kama jambo la kawaida kufuatia kuzaliwa kwa mtoto. Lakini kwa wengine wengi, ni hatua muhimu inayokosekana katika kuthibitisha utambulisho wa kisheria wa mtoto. Bila huo, watoto hawatambuliki na serikali zao, hivyo haki zao zinaweza kutolindwa na kutozingatiwa, pamoja na huduma muhimu kama huduma za afya na elimu.

Karibu robo ya watoto wote waliozaliwa duniani walio chini ya wa miaka 5 hawajawahi kusajiliwa. Maisha ya watoto hawa ni muhimu, lakini hawawezi kulindwa ikiwa serikali hawatambui.

Katika viunga vya mji mkuu wa Mauritania, Nouakchott, bustani ya mapangaboi ya kuzalisha umeme kwa njia ya upepo  yanaonekana kwa mbali na ni jawabu sahihi katika kuwa na nishati rejelezi
UNDP Mauritania/Freya Morales

Safari ya kuanzia UNFCCC hadi COP25:

Mabadiliko ya tabianchi yanatokea. Joto duniani sasa hivi ni nyuzi joto 1.1 zaidi ya ilivyokuwa mwanzoni mwa mapinduzi ya viwanda, na tayari linaleta madhara makubwa kwa ulimwengu, na kwa maisha ya watu. Ikiwa kiwango cha sasa kitazidi, basi kiwango cha joto duniani kinaweza kuongezeka kwa nyuzi joto 3.4 hadi 3.9 kwenye kipimo cha selsiyasi katika karne hii, kiwango ambacho kinaweza kusababisha madhara makubwa zaidi na yenye uharibifu kwa tabianchi.

Suala la kupoteza mtoto bado linachukuliwa kama mwiko au kitu cha aibu.
WHO/M. Purdie

Kwa nini tunahitaji kuzungumzia suala la kupoteza mtoto?

Kupoteza mtoto wakati wa ujauzito au ujauzito usio riziki bado ni jambo linaloonekana kama mwiko kulizungumzia ulimwenguni kote, mwiko unaoambatana na unyanyapaa na aibu. Wanawake wengi bado hawapati matunzo sahihi na ya heshima wanapopoteza ujauzito au kupoteza mtoto wakati wa kujifungua.

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Burundi Ezechiel Nibigira akihutubia mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74.
UN Photo/Cia Pak

Burundi yataka iondolewe kwenye ajenda ya Baraza la Usalama

Mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 ukitamatishwa hii leo  jiijni New York, Marekani, Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Burundi Ezechiel Nibigira amehutubia jukwaa hilo akitaka ajenda ya Burundi kwenye Baraza la Usalama iondolewe kwa kuwa hali ya usalama nchini humo ni tulivu.

Majengo marefu na majengo ya hoteli huko Punta Pacifica, Jiji la Panama, Panama, jiji lenye moja kati ya sekta kubwa za benki katika Amerika Kati.
World Bank/Gerardo Pesantez

Benki zenye thamani ya Dola trilioni 47 zapitisha kanuni mpya endelevu zinazoungwa mkono na UN

Maendeleo ya kiuchumi

Benki, kwa pamoja, zenye mali ya thamani ya dola trilioni 47, au theluthi ya sekta nzima kimataifa, jumapili zimetoa ahadi ya kuunga mkono kanuni mpya za benki zinazoungwa mkono na Umoja wa Mataifa ili kukuza hatua dhidi ya tabianchi na mabadiliko kutoka mifano ya ukuaji wa uchumi "wa udhurungi hadi kijani".