Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Mandhari ya milima mjini Sharm El-Sheikh, na Qesm Sharm Ash Sheikh, Misri
Unsplash/Juanma Clemente-Alloza

COP27: Unachohitaji kufahamu kuhusu mkutano mkubwa wa Mabadiliko ya Tabianchi wa Umoja wa Mataifa la mwaka huu.

Mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa Kimataifa wa tabianchi COP27 mwaka huu unafanyika huko Sharm el-Sheikh,nchini Misri wakati ambapo dunia inashuhudia ongezeko la hali mbaya ya hewa duniani kote, shida ya nishati iliyochochewa na vita vya Ukraine, na takwimu za wanasayansi zinasisitiza kwamba ulimwengu haufanyi vya kutosha kukabiliana na utoaji wa hewa ya kaboni na kulinda mustakabali wa sayari yetu.

Hussein Juma Hassan mnufaika wa mradi wa ILO wa kutambua na kurasimisha mafunzo ya awali anasema anapenda zaidi kazi ya kuchomelea vyuma katika malori na matrekta.
© ILO/OIT Belinda Japhet

Simulizi ya Hussein Juma Hassan: Kufeli masomo si kufeli maishani

Nilipopata fursa ya kusoma ili nipate cheti cha kutambuliwa rasmi kuwa mchomeleaji vyuma mwenye stadi, sikuchelea bali nilikuwa na hamu ya kuchukua fursa hiyo. Awali sikuwa na uthibitisho wa stadi hiyo na uzoefu niliokuwa nao ulitokana na kufanya kazi hii kwa miaka 25 na kujifunza nikiwa kazini. Ni simulizi ya Hussein Juma Hassan kutoka Zanzibar, Tanzania, baba wa familia ya mke na watoto 6.