Wafanyakazi wa misaada wanaokoa maisha katika hali ya hatari: Siku ya Usaidizi wa Kibinadamu Duniani
Katika Siku ya usaidizi wa kibinadamu Duniani, inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Agosti, wafanyakazi wa misaada Ahmad Alragheb, anayeishi nchini Syria, na Veronica Houser, aliyeko Afghanistan, wanazungumza kuhusu juhudi muhimu za kibinadamu katika nchi hizi, na changamoto wanazokabiliana nazo wao na wenzao.