Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Vijana Kenya wajiandaa ujumbe wao katika mkutano wa hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi
Huku dunia ikikumbwa na changamoto zinazotakana na mabadiliko ya tabianchi harakati zinafanywa kuweza kukabiliana na athari zozote ambazo zinaweza kuibuka siku za usoni.
Vijana kutoka Kenya wafanya mkutano wa maandalizi ya mkutano wa hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi
Huku dunia ikikumbwa na changamoto zinazotakana na mabadiliko ya tabianchi harakati zinafanywa kuweza kukabiliana na athari zozote ambazo zinaweza kuibuka siku za usoni.
Tunapokabiliana na mabadiliko ya tabianchi tusipuuze tabaka la Ozoni-Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema dunia inapojikita katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi basi isipuuze tabaka la Ozoni na kuwa na tahadhari ya tishio kubwa linalosababishwa na matumizi haramu ya gesi zinazotoboa tabaka la Ozoni au chlorofluorocarbons.“utambuzi wa hivi karibuni wa utoaji wa moja ya gesi hizo (CFC-11) unatukumbusha kwamba tunahitaji kuendelea na mifumo ya kufuatilia , kutoa taarifa, kuboresha na kuchukua hatua.”
Tunahitaji kukomesha mabadiliko ya tabianchi:UN
Tunahitaji kuhakikisha tunakomesha mabadiliko ya tabianchi amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres baada ya kurejea kutoka Abaco katika visiwa vya Bahama ambako kumeathirika sana na kimbinga doriani.
Shmbulio dhidi ya kituo cha mafuta Saudia linatutia hofu:Griffiths
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen Martin Griffiths amesema anatiwa hofu kubwa kuhusu mashambulio yaliyofanywa na ndege isiyo na rubani au drine katika vituo viwili vya mafuta kwenye Ufalme wa Saudi Arabia.
Akizuru visiwa vya Bahama Guterres ataka hatua zaidi dhidi ya mabadiliko ya tabianchi
Viongozi wa dunia watakaohudhuria mkutano unaokuja wa hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa wametakiwa kuja wamejizatiti sio na hotuba bali mipango ya kufikia malengo ya kupunguza hewa ukaa na kuimarisha mnepo dhidi ya changamoto hiyo ya kimataifa.
Mabadiliko ya tabianchi ni moja ya vielelezo vya wakati wetu lakini pia ni moja ya vitisho vya kiafya duniani
Mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani, WHO, Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus leo amewasihi viongozi wa wa dunia kuilinda afya dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.
Ili kuachana na utegemezi wa bidhaa ni lazima kubadili mwelekeo:UNCTAD
Mabadiliko katika uzalishaji wa bidhaa ndiyo njia bora ya kukabiliana na changamoto zinazotokana na na mabadilliko ya tabia nchi kwenye nchi zinazoendelea kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Biashara na Maendeleo la Umoja wa Matafa UNCTAD. Jason Nyakundi anatupasha zaidi
Nchi zinazoendelea lazima zibadili mwelekeo kuacha utegemezi wa bidhaa:UNCTAD
Mabadiliko katika uzalishaji wa bidhaa ndiyo njia bora ya kukabiliana na changamoto zinazotokana na na mabadilliko ya tabia nchi kwenye nchi zinazoendelea kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Biashara na Maendeleo la Umoja wa Matafa UNCTAD. Jason Nyakundi anatupasha zaidi
Rejesha ardhi katika ubora wake ili kuiokoa dunia na kukuza uchumi- Ibrahim Thiaw
Mkutano wa 14 wa nchi wanachama wa mkataba wa kuzuia kuenea kwa jangwa, UNCCD ukiendelea huko New Delhi, India, Katibu Mtendaji wa mkataba huo Ibrahim Thiaw amesema dunia sasa inatakiwa kuwekeza katika urejeshaji wa ardhi katika ubora kama njia mojawapo ya kuboresha ustawi wa maisha, kupunguza hatari za mabadiliko ya tabianchi na kupunguza hatarizinazoweza kuyumbisha uchumi.