Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Picha ya Septemba 2019 ya tabaka la ozoni rangi ya buluu na zambarau ikiashiria maeneo ya ozoni yaliyoharibika
NASA

Tunapokabiliana na mabadiliko ya tabianchi tusipuuze tabaka la Ozoni-Guterres 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema dunia inapojikita katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi basi isipuuze tabaka la Ozoni na kuwa na tahadhari ya tishio kubwa linalosababishwa na matumizi haramu ya gesi zinazotoboa tabaka la Ozoni au chlorofluorocarbons.“utambuzi wa hivi karibuni wa utoaji wa moja ya gesi hizo (CFC-11) unatukumbusha kwamba tunahitaji kuendelea na mifumo ya kufuatilia , kutoa taarifa, kuboresha na kuchukua hatua.”

Sauti
2'22"
Mabadiliko ya tabianchi na matumizi mabaya ya ardhi yamechangia katika kusababisha jangwa kwa mfano katika eneo la kaskazini mashariki mwa Cameroon (Januari 2019)
UN News/Daniel Dickinson

Rejesha ardhi katika ubora wake ili kuiokoa dunia na kukuza uchumi- Ibrahim Thiaw

Mkutano wa 14 wa nchi wanachama wa mkataba wa kuzuia kuenea kwa jangwa, UNCCD ukiendelea huko  New Delhi, India, Katibu Mtendaji wa mkataba huo Ibrahim Thiaw amesema  dunia sasa inatakiwa kuwekeza katika urejeshaji wa ardhi katika ubora kama njia mojawapo ya kuboresha ustawi wa maisha, kupunguza hatari za mabadiliko ya tabianchi  na kupunguza hatarizinazoweza kuyumbisha uchumi.