Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Kutoka kushoto: Dereva wa ambulensi akisafishwa baada ya kubeba watuhumiwa wa Ebola; Jökulsárlón Glacier Lagoon huko Iceland inazidi kuwa kutoka kwa barafu inayopungua
UN Photo.

Mwaka 2014-2016

Desemba mwaka 2013 ukifunga pazia katika kijiji cha Meliandou nchini Guinea, mtoto Emile Ouamouno alifariki. Hii ilikuwa ni pigo kubwa kwa familia yake lakini kifo hicho kilikuwa na athari zaidi baada ya Emile kutajwa kama mgonjwa wa mwanzo kabisa wa ,mlipuko mbaya zaidi wa Ebola kuwahi kushuhudiwa.

Sauti
3'59"
UN Photo.

Mwaka 2014-2016

Desemba mwaka 2013 ukifunga pazia katika kijiji cha Meliandou nchini Guinea, mtoto Emile Ouamouno alifariki. Hii ilikuwa ni pigo kubwa kwa familia yake lakini kifo hicho kilikuwa na athari zaidi baada ya Emile kutajwa kama mgonjwa wa mwanzo kabisa wa ,mlipuko mbaya zaidi wa Ebola kuwahi kushuhudiwa.

Sauti
3'59"
Mahali unakofanyika mkutano wa Umoja wa Mataifa dhidi ya mabadiliko ya tabianchi COP25 mjini Madrid, Hispania
ifema feria de madrid

Ni muhimu COP25 imalize sintofahamu ya ibara ya sita ya Mkataba wa Paris-Inger Andersen

Mkutano wa 25 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP25 ukianza hii leo mjini Madrid, Hispania, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Mpango wa mazingira wa Umoja wa Mataifa, UNEP Inger Andersen awali mjini New York Marekani kupitia mahojiano maalumu na UN News amesema moja ya vipaumbele vikuu vya mkutano huu itakuwa ni kufikia muafaka wa ibara ya sita ya mkataba wa Paris ambayo haikupata muafaka katika mkutano wa mwaka jana uliofanyika mjini Katowice Poland.

Sauti
2'4"
Mtambo wa makaa ya mawe Tuzla, Bosnia
UNEP

Bila kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa kwa asilimia 7.6 lengo la nyuzi joto 1.5 halitafikiwa-Ripoti ya UNEP

Katika kuelekea mwaka ambao mataifa yataimarisha ahadi zao za ulindaji wa hali ya hewa zilizoafikiwa mjini Paris, ripoti mpya iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi na shirika la Mpango wa mazingira wa Umoja wa Mataifa, UNEP, imeonya kuwa, ulimwengu utashindwa kufikia lengo la nyuzi joto 1.5 la mkataba wa Paris ikiwa dunia haitapunguza hewa chafuzi kwa asilimia 7.6 kila mwaka kati ya mwaka 2020 na 2030.