Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Bila kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa kwa asilimia 7.6 lengo la nyuzi joto 1.5 halitafikiwa-Ripoti ya UNEP
Katika kuelekea mwaka ambao mataifa yataimarisha ahadi zao za ulindaji wa hali ya hewa zilizoafikiwa mjini Paris, ripoti mpya iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi na shirika la Mpango wa mazingira wa Umoja wa Mataifa, UNEP, imeonya kuwa, ulimwengu utashindwa kufikia lengo la nyuzi joto 1.5 la mkataba wa Paris ikiwa dunia haitapunguza hewa chafuzi kwa asilimia 7.6 kila mwaka kati ya mwaka 2020 na 2030.
Mahitaji ya kibinadamu Sudan ni makubwa na yanatia hofu:Lowcock
Mahitaji ya kibinadamu nchini Sudan ni makubwa na yanachangiwa na sababu mbalimbali amesema mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA.
Maendeleo yanayojali mazingira ni muhimu Afrika:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa bara la Afrika kuhakikisha maendeleo yao yanakuwa safi na yanayojali mazingira.
Asante Benki ya Dunia sasa tunaweza kufungua macho yetu- Wakazi Ningxia, China
Suala la kuenea kwa jangwa ni tatizo ambalo linakumba maeneo mbalimbali duniani kutokana na sababu kadhaa ikiwemo ukataji miti hovyo, ufugaji wa kuhamahama na mabadiliko ya tabianchi. Jamii ndio huathirika zaidi kama ilivyo katika eneo moja huko nchini China ambako jangwa lilienea katika enoe kubwa na hata kusababisha wakazi kupoteza njia za kujipatia kipato, na baya zaidi upepo wa jangwani ukiambatana na vumbi ulikuwa hatari zaidi kwa macho yao. Hata hivyo Benki ya Dunia ilichukua hatua na kuleta kicheko kwa wakazi wa eneo hilo kama anavyosimulia Grace Kaneiya.
Ingawa mkataba wa CRC umefanikiwa kiasi fulani watoto masikini wanasalia nyuma:UNICEF
Katika kuelekea siku ya kimataifa ya haki za mtoto hapo Novemba 20, ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF inasema kuna mafanikio ya kihistoria yaliyopatikana kwa miaka 30 lakini bado kuna changamoto kwa watoto masikini duniani
18 NOVEMBA 2019
Miongoni mwa Habari anazokuletea Flora Nducha katika Jarida la Habari hii leo
-Miaka 30 ya mkataba wa Haki za mtoto duniani CRC, kuna mafanikio kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF lakini pia changamoto zinaendelea kwa watoto masikini
-Muungano wa Afrika AU na shirika la afya duniani WHO waanzisha ubia mpya ili kushirilkiana katika kutimiza malengo ya afya
-Wakimbizi Sudan Kusini wasema wameambiwa amani imerejea Yambio sasa wanaanza kurejea nyumbani je nini wanakikuta huko?
Miaka 30 ya haki za mtoto kuna mafanikio lakini changamoto ni kubwa kwa masikini:UNICEF
Katika kuelekea siku ya kimataifa ya haki za mtoto hapo Novemba 20, ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF inasema kuna mafanikio ya kihistoria yaliyopatikana kwa miaka 30 lakini bado kuna changamoto kwa watoto masikini duniani
Nyenzo mpya ya FAO kusaidia mazao aina mabalimbali kushamiri
Nyenzo mpya ya shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO, itawajengea mnepo wakulima na kulinda mazao kwa kwa kusaidia katika uendelezaji wa kilimo cha mazao mbalimbali na pia kuwasaidia wakulima kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kuenzi mbinu za kiasili na mifumo ya kilimo.
Milima ni muhimu katika mabadiliko ya tabianchi na mnepo wa majanga:WMO
Milima mirefu zaidi duniani kuanzia Andes hadi Alps na ukanda wa milima Himalaya-Hindu Kush na Tibet hadi maeneo ya kitropiki imeathirika vibaya na mabadiliko ya tabianchi na athari hizo sasa zinashuka chini kwenye baadhi ya maeneo yenye idadi kubwa ya watu duniani.
Milima ni muhimu katika mabadiliko ya tabianchi na mnepo wa majanga:WMO
Milima mirefu zaidi duniani kuanzia Andes hadi Alps na ukanda wa milima Himalaya-Hindu Kush na Tibet hadi maeneo ya kitropiki imeathirika vibaya na mabadiliko ya tabianchi na athari hizo sasa zinashuka chini kwenye baadhi ya maeneo yenye idadi kubwa ya watu duniani.