Ingawa kuna changamoto najitahidi kutunza familia yangu- Tsinduka
Hii leo ni siku ya kimataifa ya familia duniani ambapo maudhui ya mwaka huu ni mienendo ya makundi ya watu na familia wakati huu ambapo idadi ya watu inaongezeka ingawa kwa kiwango cha chini. Umoja wa Mataifa unasema kupungua kwa idadi ya wanafamilia hutoa fursa ya familia kupatia huduma bora zaidi watoto, mathalani elimu na afya.