Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN Women/Luke Horswell

UNFPA Kenya yaeleza mipango yake ya kutetea haki za wanawake

Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Umoja wa Mataifa la afya ya uzazi na idadi ya watu UNFPA nchini Kenya Anders Tomsen, ameeleza shirika hilo linatekeleza ipasavyo tamko la Umoja wa Mataifa la haki za binadamu ambalo mwaka huu linafikisha miaka 75 hususan ibara ya Tano ambayo inasema Haki ya mtu ya kwamba asitumbukizwe kwenye vitendo vya mateso, ukatili, au adhabu dhalili.

Akihojiwa na mwandishi wetu wa Kenya Thelma Mwadzaya Tomsen anaanza kwa kusema shirika hilo limeundwa kwa kuzingatia misingi ya haki. 

Sauti
3'2"
UN News/George Musubao

Wananchi wahamasishwa kuyalinda mazingira baada ya mafuriko Kalehe, DRC.

Muungano wa mashirika ya kiraia katika eneo la Kalehe jimboni Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wako katika harakati za kuhamasisha wananchi kupanda miti na kuchukua hatua nyingine zitakazosaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi baada ya eneo hilo kukumbwa na mafuriko yaliyosababisha vifo na uharibifu mkubwa mapema mwezi Mei Mwaka huu. Mwandishi wetu wa DRC George Musubao amefika huko na kutuandalia makala ifuatayo. Kwako George.

Sauti
4'38"
UNAMA / Eric Kanalstein

Mariam: Dawa za kulevya zilinifanya kupoteza mtoto na mume

Tatizo la dawa za kulevya duniani ni suala tata ambalo linaathiri mamilioni ya watu duniani kote. Watu wengi wanaotumia dawa za kulevya hukumbana na unyanyapaa na ubaguzi, jambo ambalo linaweza kudhuru zaidi afya yao ya kimwili na kiakili na kuwazuia kupata usaidizi wanaohitaji.

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na Dawa za Kulevya na Uhalifu UNODC inatambua umuhimu wa kuchukua mtazamo unaozingatia watu kuhusu sera za dawa za kulevya, kwa kuzingatia haki za binadamu, huruma na mazoea yanayotegemea ushahidi. 

Sauti
4'1"
Maktaba ya Kibinafsi/Zepline Ouma

Fahamu Umuhimu wa yoga katika kujenga mwili

Aina nyingi za mazoezi zinaweza kusaidia kuimarisha maisha yako, lakini hapa tunazingatia zoezi ya yoga kwa sababu ni wiki hii tarehe 21 Juni ambapo ulimwengu umeazimisha siku ya Yogan Duniani.

Maudhui ya mwaka huu ya siku hii “Yoga kwa ajili ya ustawi wa sayari moja, familia moja.” 

Kufahamu zoezi hii kwa undani pamoja na faida zake mwilini, tunamsikiliza mwalimu wa Yoga kutoka Kenya Zepline Ouma.

Sauti
2'26"
Hamad Rashid

Mradi wa ALiVE awamu ya pili kupima stadi za watoto nje ya masomo ya kawaida Zanzibar

Baada ya kufanya tathmini ya upimaji Stadi za maisha na maadili kwa vijana wenye umri wa miaka 13  hadi 17 nchini Kenya, Uganda na Tanzania, mradi wa ALiVE katika awamu ya pili umepanga kuwafikia watoto wenye umri wa miaka  6  hadi 12 ambao bado wako shule ili kuwapima viwango vyao vya Stadi za maisha na maadili ikiwa ni katika jitihada za kuchechemua fikra tunduizi na kusongeza malengo ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu, SDGs. 

Sauti
5'34"
UN News / Thelma Mwadzaya

Viwavi jeshi vimerejea Afrika Mashariki, FAO kusaidia kuvikabili

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO, limetahadharisha kuwa viwavijeshi ambavyo vimeripotiwa kuonekana kwenye mbuga na hifadhi za wanyama nchini Kenya vimerejea.Wadudu hao pia wameonekana kwenye mataifaJirani ya Eritrea, Sudan Kusini,Ethiopia, Somalia na Uganda. Ifahamike kuwa mwaka 2016 viwavijeshi vilionekana kwenye mataifa 6 pekee barani Afrika.Viwavijeshi vina uwezo wa kuvamia na kukomba mazao ya mahindi, ngano, mtama, shayiri na nyasi. Kwa undani zaidi wa juhudi hizo ungana na mwandishi wetu wa Kenya Thelma Mwadzaya katika Makala hii.

Sauti
3'48"
TMA/Eugene Uwimana

WMO kuimarisha mifumo ya tahadhari ya mapema dhidi ya majanga Afrika Mashariki

Shirika la Umoja wa Mataifa la hali ya hewa duniani WMO kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupunguza hatari za majanga UNDRR wiki hii wamezindua mradi mpya wa kuimarisha mifumo ya tahadhari ya mapema ya kikanda. Mradi huo uliopewa jina “Kuimarisha huduma za hali ya hewa na tahadhari ya mapema katika Ukanda wa Afrika Mashariki” utafanya kazi katika nchi sita za ukanda huo ambazo ni Kenya, Tanzania, Rwanda, Uganda, Burundi na Sudan Kusini.

Sauti
4'10"
Hamad Rashid

Taasisi 16 zakutana Morogoro Tanzania kusongesha SDG 4

Taasisi 16 zikiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali, asasi za kiraia na vyuo vikuu ambao kwa pamoja ni wanachama wa Mtandao wa Elimu Afrika Mashariki (RELI) wamekutana mjini Morogoro, Tanzania kujengewa uwezo wa namna ya kuimarisha juhudi za kuchochea mabadiliko ya elimu na kuhamasisha ujengaji fikra tunduizi kwa vijana ili kusongesha lengo namba 4 la Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu SDGs.

Sauti
5'10"
TANBAT 6/Kapteni Mwijage Inyoma

TANBAT 6, walinda amani wa UN kutoka Tanzania wapokea pongezi kutoka JWTZ na MINUSCA

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa Kikosi cha 6 cha kutoka Tanzania TANBAT 06 wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA) wamepokea ugeni na salamu kutoka Jeshi la Ulinzi wa Wananchi Tanzania (JWTZ) kupitia ujumbe uliongozwa na Brigedia Jenerali George Mwita Itang’are aliyewakilisha salamu za Mkuu wa Majeshi ya Tanzania kutokana na sifa nzuri anazozipokea kutoka MINUSCA kuhusu kikosi hicho. Afisa Habari wa TANBAT 06 Kapteni Mwijage Inyoma ameshiriki na kutuandalia makala hii..

Sauti
3'26"