Uhifadhi wa kompyuta au simu wachangia uhifadhi wa mazingira Burundi
Kawaida likija swala la kuhifadhi mazingira , katika nchi zinazoendelea watu hufikiria haraka swala la mabadiliko ya tabia nchi na uchafuzi wa hewa ikiwemo uhifadhi wa miti , mito na kadhalika. lakini je unajua kuwa uhifadhi wa komputa au simu ni moja ya mikakati ya kuhifadhi vyema mazingira? Nchini Burundi , sehemu nyingi na ofisini hamna utaratibu wa kuhifadhi komputa na simu za mikononi au rununu, na hivyo hali hiyo kuonekena kama ni kitisho kikubwa cha mazingira na afya.