Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Milima yazidi kuporwa, maisha ya wakazi wake yazidi kuwa duni

Milima ni tegemeo la wakazi wa dunia kwa shughuli na huduma mbali mbali ikiwemo maji ya kunywa, umwagiliaji, shughuli za kiuchumi ikiwemo utalii na kadhalika. Hata hivyo maendeleo ya binadamu yamekuwa kikwazo kwa milima kuweza kutoa huduma hizo na hata kuhatarisha maisha ya wakazi au jamii za milimani. Katika siku ya kimataifa ya milima duniani hii leo tarehe 11 Disemba 2012 inaelezwa kuwa milima iko hatarini zaidi hivi sasa na hata maisha ya wakazi wa milimani nayo yanazidi kuwa duni. Je ni kwa nini?

Hadhi mpya ya Palestina ndani ya Baraza Kuu la UM kuchochea amani Mashariki ya Kati

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi tarehe 29 Novemba ambayo ni siku ya kimataifa ya kusimama bega kwa bega na Palestina, lilipitisha azimio la kuipatia Palestina hadhi ya uangalizi bila haki ya kupiga kura katika Baraza hilo.

Katika kura hiyo ya kupitisha azimio hilo, nchi 138 ziliunga mkono huku Tisa zikipinga na nchi 41 zikiwa hazikuonyesha msimamo wowote. Nchi zilizopiga kura ya hapana ni pamoja na Marekani na Israeli huku Uingereza na Hungary zikiwa miongoni mwa nchi ambazo hazikuonyesha msimamo wowote.

Madhara ya mabadiliko ya hali ya hewa yaweza kuwa kichocheo cha kudhibiti utoaji gesi chafuzi

Mkutano wa mabadiliko ya hali ya hewa unafanyika Doha, Qatar suala kubwa likiwa ni hatua za kuchukua kupunguza gesi chafuzi zinazochochea ongezeko la joto duniani. Wakati hilo likijdaliwa, shirika la mpango wa Mazingira katika Umoja wa Mataifa, UNEP, limetoa taarifa inayozungumzia uwezekano wa kuyeyuka kwa kasi kubwa kwa udongo wenye barafu, Permafrost, ulioko kwenye maeneo ya kaskazini mwa dunia kitendo ambacho kitatoa hewa aina ya Methani yenye madhara zaidi kwa dunia kuliko hewa ya ukaa.

Kampeni ya 'Mimi pia ni mhamiaji', Afrika Kusini: IOM

Nchini Afrika kusini, Shirika la Uhamiaji la kimataifa, IOM kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wanaanzisha kampeni iitwayo, Mimi pia ni mhamiaji yenye lengo la kuhamasisha raia wa nchi hiyo wafahamu kuwa wahamiaji nao pia ni sehemu ya jamii yao na hivyo kuleta utangamano miongoni mwa wakazi wote.

Kampeni hiyo itaendelea hadi tarehe 18 mwezi ujao ambayo ni siku ya kimataifa ya wahamiaji, ikijikita zaidi kuelimisha kuwa kimsingi raia wote wa Afrika Kusini ni wahamiaji au wana uhusiano na wahamiaji.

Kongamano la utalii barani Afrika laanza nchini Tanzania

Wataalamu wa masuala ya utalii barani afrika leo wanaanza kongamano la siku tano nchini Tanzania ambalo pamoja na mambo mengine linatazamiwa kujadilia usimamizi wa utalii endelevu katika hifadhi za taifa.

Kongamano hilo ambalo limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Tanzania na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na utalii linahudhuriwa na wajumbe zaidi ya 400 kutoka barani afrika na nje ya bara hilo.

Kutoka DSM, Mwandishi wetu George Njogopa ameaandaa taarifa ifuatayo.

Gurudumu la mabadiliko Somalia halirudi tena nyuma: Balozi Mahiga

Nchi ya Somalia imepongezwa na viongozi kadha wa kadha, akiwemo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ban Ki-Moon, kutokana na jitihada ambazo imepiga kwenye mabadiliko ya kisiasa.

Katika hali hiyo, viongozi hawa wametoa wito kwa jamii ya kimataifa kuendelea kuiunga mkono Somalia, kwani bado inakabiliwa na changamoto za kibinadamu na za kiusalama. Tangu kuteuliwa kama Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Somalia, Balozi Augustine Mahiga amefanya kazi kwa bidii kuhakikisha kwamba Somalia imefikia kwenye nafasi iliyoifikia sasa.

Mshindi wa hotuba ya Katibu Mkuu kutoka Kenya ataka vijana wawe na usemi zaidi

Wallace Chwala, mwanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi Kenya, ni mmoja wa washindi wa uandishi wa mfano wa hotuba ambayo ingetolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, wakati wa kufungua kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Shindano hilo la uandishi wa hotuba ya Katibu Mkuu, liliandaliwa na Taasisi ya Brookins kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa, na ikawashirikisha vijana kutoka kote duniani. Washindi walialikwa mjini New York kukutana na Katibu Mkuu, Ban Ki-Moon kwenye Siku ya Kimataifa ya Amani.