Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Milima yazidi kuporwa, maisha ya wakazi wake yazidi kuwa duni

Milima yazidi kuporwa, maisha ya wakazi wake yazidi kuwa duni

Pakua

Milima ni tegemeo la wakazi wa dunia kwa shughuli na huduma mbali mbali ikiwemo maji ya kunywa, umwagiliaji, shughuli za kiuchumi ikiwemo utalii na kadhalika. Hata hivyo maendeleo ya binadamu yamekuwa kikwazo kwa milima kuweza kutoa huduma hizo na hata kuhatarisha maisha ya wakazi au jamii za milimani. Katika siku ya kimataifa ya milima duniani hii leo tarehe 11 Disemba 2012 inaelezwa kuwa milima iko hatarini zaidi hivi sasa na hata maisha ya wakazi wa milimani nayo yanazidi kuwa duni. Je ni kwa nini? Assumpta Massoi wa Radio ya Umoja wa Mataifa amezungumza na Richard Muyungi Mwenyekiti wa Kamati ya dunia ya kisayansi na Taaluma ya mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi.