Balozi Mahiga awasihi wabunge wa Somalia kuendeleza upeo ulofikiwa sasa kisiasa Somalia
Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Somalia, Augustine Mahiga, amewasihi wabunge katika bunge jipya la Somalia kutumia fursa na wadhfa walio nao ili kuweka msingi bora kwa ajili ya siku za baadaye za taifa hilo la Pembe ya Afrika, wakati wa kumchagua rais mpya mnamo siku ya Jumatatu Septemba 10.