Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

06 SEPTEMBA 2022

Katika Jarida la mada kwa kina hii leo Flora Nducha anakuletea

-Mashirika ya misaada ya kibinadamu yamesema Somalia imefikia kkatika hali mbayá sana. Maisha ya mamia ya maelfu ya watu yamo hatarini hivi sasa kutokana na tathimini iliyofanywa hivi karibuni kuhusu uhakika wa chakula na lishe. Baa la njaa linajitokeza katika wilaya za Baidoa na Burkhakaba kwenye jimbo la Bay lina uwezekano wa kudumu hadi Machi 2023 ikiwa msaada wa kibinadamu hautaongezwa kwa kiasi kikubwa na mara moja.

Sauti
11'51"

02 Septemba 2022

Ungana na Flora Nducha anayekuletea jarida kutoka kila kona ya dunia na kuanzia huko Pakistan

- Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanafanya kila juhudi kuhakikisha yanasaidia zaidi ya watu milioni 33 walioathirika na mafuriko nchini Pakistan baada ya mvua za monsoon kunyesha kwa kiwango kikubwa sana na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 1200 huku yakiharibu kabisa miundo mbinu mingine. 

Sauti
12'23"

01 SEPTEMBA 2022

Katika Jarida la mada kwa kina hii leo Flora Nducha anakuletea

-Msimu mpya wa shule ukianza sehemu mbalimbali duniani , takwimu mpya zilizotolewa leo mjini Paris Ufaransa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO zinaonyesha kwamba watoto na vijana milioni 244 wenye umri wa kati ya miaka 6 na 18 duniani kote bado hawako shule.

-Mkuu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths leo ameanza ziara nchini Somalia kushuhudia hali halisi ya njaa na kutathimini mahitaji ya walioathirika na ukame na hatua zinazochukuliwa kuwasaidia.

31 AGOSTI 2022

Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea 

-Leo ni siku ya kimataifa ya watu wenye asili ya Afrika, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anasema licha ya mchango wao mkubwa bado wanaendfelea kubaguliwa kote duniani.

-Meli iliyosheheni msaada wa chakula kilichonunuliwa na shirika la mpango wa chakula duniani WFP kutoka nchini Ukraine kwenda Ethiopia imetia nanga jana nchini Djibout tayari kusambazwa kwa msaada huo

Sauti
10'50"

30 AGOSTI 2022

Katika jarida la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea 

-Nusu ya vituo vya huduma za afya duniani kote vinakosa huduma za usafi na hivyo kuwaweka wagonjwa na wahudumu wa afya katika hatari kubwa ya kusambaza magonjwa na maambukizi kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa leo na WHO na UNICEF.

Sauti
12'56"

29 AGOSTI 2022

Flora Nducha anakuletea jarida lililo sheheni habari mbalimbali kuanzia nchini Ethiopia ambapo tume ya Kimataifa ya wataalamu wa Haki za binadamu nchini Ethiopia imekasirishwa na kuzuka upya kwa uhasama kati ya serikali ya Ethiopia na chama cha Tigray People's Liberation Front tangu wiki iliyopita na kuzitaka pande zote mbili kurudi kwenye meza ya mazungumzo kwani wanaoteseka ni raia.

Wakimbizi wa Burundi wakioko katika kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma nchini Tanzania wameshukuru kwa watoto wao kupatiwa vyeti vya kuzaliwa 

Sauti
10'26"

26 AGOSTI 2022

Katika Jarida la habari za UN hii leo Flora Nducha anakuletea -Mradi wa maji safi na salama jimboni Cibitoke nchini Burundi kwa msaada wa UNICEF umeleta afuweni kwa wakazi na hasa watoto -Mkimbizi kutoka DRC anayeishi Kakuma Kenya ameleta nuru ya nishati ya sola kwa wakimbizi wenzie huku akijiingizia kipato -Makala leo inatupeleka Tanzania kumulika jitihada za vijana katika kupambana na ukimwi na afya ya uzazi kwa kuelimisha vijana Balehe -Na mashinani afisa wa shirika la afya duniani WHO nchini Senegal anaeleza changamoto za upatikanaji wa taarifa za afya Afrika
Sauti
11'51"

25 AGOSTI 2022

Katika Jarida la Umoja wa Mataifa la mada kwa kina hii leo Flora Nducha anakuletea

-Ni miaka mitano tangu kuzuka kwa mgogoro wa Rohingya nchini Myanmar ambapo mamilioni walilazimika kufungasha virago na wengi kuingia nchini Bangladesh, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema takribani milioni 1 bado ni wakimbii na 150,000 wanaishi makambini Rakhine Bangladesh

Audio Duration
12'43"

24 AGOSTI 2022

Katika Jarida la habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Ni miei sita tangu kuzuka kwa vita nchini Ukraine, mashirika ya Umoja wa Mataifa yamefanya nini hadi sasa kuwasaidia wananchi wa taifa hilo?
-Nchini Sudan Kusini mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani UNMISS umejenga shule na kituo cha polisi mjini Mvolo katika jitihada za ujenzi wa amani

Sauti
11'45"

23 AGOSTI 2022

Katika Jarida la habari la Umoja wa Mataifa hii leo , Flora Nducha anakuletea

-Mlipuko mpya wa Ebola wazuka Kivu Kaskazini baada ya mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 46 kufariki dunia na kuthibitishwa kuwa alikuwa na virusi vya Ebola kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO

Sauti
11'33"