06 SEPTEMBA 2022
Katika Jarida la mada kwa kina hii leo Flora Nducha anakuletea
-Mashirika ya misaada ya kibinadamu yamesema Somalia imefikia kkatika hali mbayá sana. Maisha ya mamia ya maelfu ya watu yamo hatarini hivi sasa kutokana na tathimini iliyofanywa hivi karibuni kuhusu uhakika wa chakula na lishe. Baa la njaa linajitokeza katika wilaya za Baidoa na Burkhakaba kwenye jimbo la Bay lina uwezekano wa kudumu hadi Machi 2023 ikiwa msaada wa kibinadamu hautaongezwa kwa kiasi kikubwa na mara moja.