31 AGOSTI 2022
Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Leo ni siku ya kimataifa ya watu wenye asili ya Afrika, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anasema licha ya mchango wao mkubwa bado wanaendfelea kubaguliwa kote duniani.
-Meli iliyosheheni msaada wa chakula kilichonunuliwa na shirika la mpango wa chakula duniani WFP kutoka nchini Ukraine kwenda Ethiopia imetia nanga jana nchini Djibout tayari kusambazwa kwa msaada huo
-Makala yetu inatupeleka wilayani Mbinga mkoani Ruvuma Tanzania ambako mtadi wa nishati ya maji wa AHEPO unaofadhiliwa na shirika la mitaji la Umoja wa Mataifa UNCDF umeleta mabadiliko kwa jamii
-Na mashinani utamsikia mwanzilishi wa kikundi cha kina mama watengeneza vikapu mkoani Iringa na Njombe Tanzania akieleza jinsi wanavyojikimu kimaisha na mradi huo huku wakilinda mazingira