21 SEPTEMBA 2022
Katika Jarida la habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Kandoni mwa mjadala wa wazi wa Umoja wa Mataifa shirika la afya duniani WHO limewataka viongozi wa dunia kuchukua hatua haraka kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza NCDs yanayokatili maisha ya watu milioni 50 kila mwaka
-Kijana Mtanzania Gibson Kawago ni miongoni mwa vijana 17 waliotangazwa leo na Umoja wa Mataifa kuwa viongozi vijana wa kusongesha malengo ya maendeleo endelevu SDG's je amepokeaje uteuzi huo na anapanga kufanya nini?