Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

20 Oktoba 2021

Karibu uungane na Assumpta Massoi akikuletea mada kwa kina mahsusi ikimulika harakati za Umoja wa Mataifa za kuimarisha afya na kuinua kipato mashinani. 

Pia utapata fursa ya kusikia habari kwa ufupi zikieleza kuuawa kwa watoto nchini Syria katika Shambulio, msaada wa kibinadamu kwa nchi ya Madagascar na mkutano wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa unaoongozwa na Kenya. 

 

Audio Duration
9'54"

19 Oktoba 2021

Hii leo ASSUMPTA MASSOI  anakujuza mengi ikiwemo, watu mashuhuri 34 wanapanda mlima Kilimanjaro ili kuchagiza usawa wa chanjo ya COVID-19. Mkataba wa amani Sudan Kusini bado kitendawili kwa wakazi wa Tambura. Na nchini Tanzania vijana wajasiriamali katika mkoa wa Singida wameitikia wito wa Umoja wa Mataifa wa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, TEHAMA kama njia mojawapo ya kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu, SDG hususan kipengele cha teknolojia cha lengo namba 17 la kuimarisha mbinu za utekelezaji wa malengo na kuchochea ubia wa kimataifa

Audio Duration
14'29"

18 Oktoba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo baada ya kusikiliza habari kwa ufupi utasikia mada kwa kuhusu chakula cha asili kutoka Kilimanjaro nchini Tanzania.

Mwishoni mwa wiki dunia imeadhimisha siku ya chakula duniani ikibeba maudhui “Hatua zetu ndio mustakbali wetu” kwa ahadi ya kuimarisha mifumo ya chakula na kuhakikisha watu wote mahali popote walipo duniani wanapata lishe bora na mlo kamili. 

Sauti
11'10"

15 Oktoba 2021

Ni Ijumaa ya tarehe 15 mwezi Oktoba mwaka 2021 siku ya kimataifa ya wanawake wa vijijini.

Karibu uungane na Flora Nducha kusikiliza jarida ambapo kama ilivyo ada ijumaa ni siku ya kuwa na mada kwa kina na hii leo tunamulika afya ya akili tukifunga safari hadi Kenya kwa msichana aliyetaka kujiua, kulikoni? 

Pia utapata fursa ya kujifunza lugha ya Kiswahili ambapo leo tunapata ufafanuzi wa maana za neno "KITAMBI" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania , BAKITA.

Sauti
17'31"

14 OKTOBA 2021

Katika Jarida la Habari za UN hii leo Assumpta Massoi anakuletea

-Janga la corona au COVID-19 limerudisha nyuma jitihada za kutokomeza kifua kikuu au Tb limeonya shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO

-Kuelekea siku ya wanawake wa kijijini hapo kesho Oktoba 15 utawasikia wanawake kutoka Tanzania wakielezea changamoto za COVID-19 katika kujikimu kimaisha

-Takwimu mpya zionaonyesha wagonjwa wa COVID-19 wamepungua lakini bado kuna nchi kama Burundi na Korea Kaskazini hazijaanza kutoa chanjo dhidi ya gonjwa hilo

Sauti
15'59"

13 Oktoba 2021

karibu usikilize jarida maalum ambapo leo tunakuletea mada kwa kina tukikupeleka nchini Uingereza kwa mwandishi wa vitabu Abdulrazak Gurnah mshindi wa tuzo ya Nobel ya mwaka 2021 katika fani ya Fasihi. 

Tuzo ya Nobel ilianza kutolewa mwaka 1901 na kamati ya tuzo ya amani ya nobel ya Norway, huwatunukia tuzo pia washindi wengine katika fani za Fizikia, Fiziolojia na madawa, Falsafa, Fasihi na uchumi.

Sauti
15'55"

Jarida 12 Oktoba 2021

Karibu usikilize jarida linaloletwa kwako na Assumpta Massoi ambapo miongoni mwa utakayo sikia ni pamoja na wakulima nchini Kenya wanufaika na mradi wa viazi lishe chini ya ufadhili wa WFP. 

Binti Raba Hakim mkimbizi kutoka Ethiopia aanza masomo ya chuo kikuu kwa ufadhili wa Mastercard Foundation, na nchini Niger wakulima wapewa mafunzo ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. 

Pia utasikia makala na sauti kutokana mashinani.

Sauti
11'32"

11 Oktoba 2021

Karibu kusikiliza jarida ikiwa leo tarehe 11 mwezi Oktoba mwaka 2021 ni siku ya mtoto wa kike duniani.

Kama ilivyo ada jumatatu ni siku ya mada kwa kina ambapo leo tunakwenda nchini Tanzania kumulika huduma za posta kwa kutambua kuwa mwishoni mwa wiki ilikuwa siku ya posta duniani. 

Ungana na Flora Nducha anayekuletea jarida 

Sauti
12'13"

08 OKTOBA 2021

Katika jarida la mada kwa kina hii leo Assumpta Massoi anakuletea

-Waandishi wa habari Maria Ressa raia wa Ufilipino na Dimitry Muratov raia wa Urusi wameshinda tuzo ya amani ya Nobel mwaka huu 2021

-Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la mpango wa chakula duniani WFP, la elimu sayansi na utamaduni UNESCO na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wamewapongeza na kuwamwagia sifa washindi hao kwa mchango wao katika kusongeza njia ya amani

Sauti
21'4"

07 OKTOBA 2021

Jaridani hii leo Assumpta Massoi anaanza na taarifa kuhusu umaskini wa kila hali ukimulika hali ya kiafya, kielimu na kiwango cha maisha! Watu wa makabila fulani katika baadhi ya nchi ni hohehahe! Kisha ni taarifa kuhusu uamuzi wa kuruhusu matumizi ya chanjo ya Malaria barani Afrika na bila kusahau leo ni siku ya pamba duniani! Je nguo uliyovaa ni ya pamba? Makala tunabisha hodi Uganda kumulika mradi wa Benki ya Dunia wa ujenzi wa masoko na hatimaye mashinani tukisalia huko huko Uganda na hatua za kujikinga na majanga. Karibu!

Sauti
13'54"