19 Oktoba 2021
Pakua
Hii leo ASSUMPTA MASSOI anakujuza mengi ikiwemo, watu mashuhuri 34 wanapanda mlima Kilimanjaro ili kuchagiza usawa wa chanjo ya COVID-19. Mkataba wa amani Sudan Kusini bado kitendawili kwa wakazi wa Tambura. Na nchini Tanzania vijana wajasiriamali katika mkoa wa Singida wameitikia wito wa Umoja wa Mataifa wa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, TEHAMA kama njia mojawapo ya kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu, SDG hususan kipengele cha teknolojia cha lengo namba 17 la kuimarisha mbinu za utekelezaji wa malengo na kuchochea ubia wa kimataifa
Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
14'29"