Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

07 OKTOBA 2021

07 OKTOBA 2021

Pakua

Jaridani hii leo Assumpta Massoi anaanza na taarifa kuhusu umaskini wa kila hali ukimulika hali ya kiafya, kielimu na kiwango cha maisha! Watu wa makabila fulani katika baadhi ya nchi ni hohehahe! Kisha ni taarifa kuhusu uamuzi wa kuruhusu matumizi ya chanjo ya Malaria barani Afrika na bila kusahau leo ni siku ya pamba duniani! Je nguo uliyovaa ni ya pamba? Makala tunabisha hodi Uganda kumulika mradi wa Benki ya Dunia wa ujenzi wa masoko na hatimaye mashinani tukisalia huko huko Uganda na hatua za kujikinga na majanga. Karibu!

Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
13'54"