UNICEF yaisaidia DRC katika mafuriko mabaya kuhushudiwa kwa miaka 60
Mjini Kinshasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na wadau wengine wa misaada ya kibinadamu wamesema wanafanya kila liwezekanalo kuwasaidia waathirika wa mafuriko mabaya zaidi nchini humo yaliyosababisha kina cha mto Congo kufurika katika kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa katika kipindi cha zaidi ya miaka 60.