Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Mtoto mdogo akipokea matibabu katika kituo cha matibabu ya kipindupindu huko Kivu Kaskazini, DR Congo.
© UNICEF/Jospin Benekire

UNICEF yaisaidia DRC katika mafuriko mabaya kuhushudiwa kwa miaka 60

Mjini Kinshasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na wadau wengine wa misaada ya kibinadamu wamesema wanafanya kila liwezekanalo kuwasaidia waathirika wa mafuriko mabaya zaidi nchini humo yaliyosababisha kina cha mto Congo kufurika katika kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa katika kipindi cha zaidi ya miaka 60.

Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na wa Misaada ya Kibinadamu Bruno Lemarquis alipozuru DRCongo mapema Machi
© UNOCHA

Pande zinazozozana mashariki mwa DRC zakumbushwa wajibu wa kulinda raia

Mratibu wa Misaada ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Bruno Lemarquis, ameonesha wasiwasi mkubwa kuhusu ghasia zinazoongezeka katika mji wa Mweso, ulioko takribani kilomita 100 kutoka Goma, katika jimbo la Kivu Kaskazini (mashariki mwa DRC), Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewaeleza Waandishi wa habari jijini, New York Marekani.

Wakazi wa kambi ya wakimbizi wa ndani ya Bulengo jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wakiwa kwenye tamasha la mpira wa soka lililoandaliwa na Shirikisho la Soka barani Afrika, na kufanikishwa na WFP.
© WFP/Michael Castofas

Afcon: Shamrashamra zagubikwa na ukimbizi na njaa mashariki mwa DRC

Huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC shamrashamra za mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika, Afcon yanayoendelea huku Côte d'Ivoire zinagubikwa na ukimbizi na ongezeko la matukio ya ukatili wa kingono huku shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP likichukua maamuzi magumu kutokana na ukata unaokabili operesheni zake. 


 

Bi. Keita akizungumza na wanahabari huko Kalehe, Kivu Kusini.
MONUSCO/Michael Ali

MONUSCO yaafikiana na serikali ya DRC mikakati ya kuondoka nchini humo

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na Mkuu wa wa mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSC, Bi Bintou Keita na Naibu Waziri Mkuu, na Waziri wa Mambo ya nje Francophonie Christophe Lutundula walithibitisha jana Jumamosi Januari 13, dhamira ya vyombo hivyo viwili kufanya kazi kwa pamoja kwa mchakato wa kuondoka kwa MONUSCO nchini DRC kwa njia ya maendeleo, kuwajibika, heshima na kwa MONUSCO kuwa mfano wa kuigwa.